Wednesday, August 28, 2019

WIMBO WA DIAMOND NA RAYVANNY WA TETEMA KAMA UMEPIGWA SHOTI "WALETA SHOTI KENYA":


NA K-VIS BLOG
WIMBO wa “Tetema kama umepigwa shoti” ulioimbwa kwa ushirikiano kati ya mwanamuziki nyota barani Afrika Diamond Platnamz na Rayvanny (pichani juu) umezua gumzo nchini Kenya baada ya Mamlaka ya nchi hiyo kuupiga marufuku kuimbwa maeneo ya wazi (hadharani).
Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Filamu Nchini Kenya, Dkt. Ezekiel Mutua amsema kuwa ni jambo la kusikitisha kuwa hata viongozi wa kitaifa wamekuwa wakiimba na kucheza wimbo huo wa Tetema  licha ya kuwa na maudhui yenye kuvunja maadili ya Wakenya.
“Inasikitisha hata viongozi wetu wa kitaifa wamekuwa wakiimba na kucheza nyimbo za Tetema na Wamlambez hadharani, sasa nyimbo hizi  zimepigwa marufuku kuimbwa nje ya Klabu (clubs) na Baa, zinaujumbe (maudhui) machafu na hazifai  kwa matumizi ya umma hazifai kutazamwa na watoto na kiukweli zinahamasisha ngono.” Alisema Dkt. Mutua kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii za Tweetter na Facebook Agosti 27, 2019.
Hata hivyo katazo hilo la Dkt. Mutua, limezua mtiririko wa maoni kutoka kwa Wakenya wengi wakisema katazo lake limechelewa na ndio limechagiza wimbo huo kuwa maarufu miongoni mwa
Dkt. Ezekiel Mutua
Wakenya.
Kwenye ukurasa wa Facebook wa Dkt. Mutua leo asubuhi Agosti 28, 2019, jumla ya maoni 580 yametolewa huku mengi ya maoni hayo yakimweleza kuwa amechelewa kutoa tangazo hilo na kwamba hivi sasa wimbo huo umekuwa maarufu kama kama wimbo wa taifa wa Kenya.
Katika akaunti yake ya Tweetter, wasomaji 890 wamejibu ujumbe wake (tweet) na kumnekuwa na maoni mchanganyiko mengi yakimkejeli kwa katazo lake hilo.

No comments :

Post a Comment