Sunday, August 4, 2019

WAZIRI DKT. KALEMANI AZINDUA MRADI WA REA III KWA MAENEO YA PEMBEZONI MWA MIJI HUKO KIGAMBONI DAR ES SALAAM


 Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani (watatu kushoto), akiwa na Naibu Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Kigamboni, Mhe. Dkt.Faustin Ndungulile (wapili kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Mhe. Ruth Msafiri na viongozi wengine, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa REA III kwa maeneo yaliyo pembezoni mwa miji,. Uzinduzi huo ulifanyika Kigamboni Agosti 2, 2019.

 Dkt. Kalemani akizindua mradi huo huku akiwa na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustin Ndungulile (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Ruth Msafiri.
 Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, akihutubia wananchi wakati wa uzinduzi huo.
 Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, akihutubia wananchi wakati wa uzinduzi huo.
 Dkt. Kalemani (kulia), akipungia mkono wananchi huku akionbgozana na Naibu Waziri wa Afya ambaye pia ni Mbunge wa Kigamboni, Dkt. Faustin Ndungulile (katikati).
 Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam, Mhe. Ruth Msafiri akihutubia wakati wa uzinduzi huo.

Dkt. Kalemani akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Ruth Msafiri
NA K-VIS BLOG
WAZIRI wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, amezindua Mradi wa REA awamu ya III kwa  Wilaya zilizo pembezoni mwa Miji ikiwemo Wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Uzinduzi huo umefanyika Agosti 2, 2019 huko Kigamboni ambapo Mhe. Dkt. Kalemani amemuagiza mkandarasi kumaliza kazi kwa wakati kama ambavyo mkataba unavyoeleza.
Dkt. Kalemani amesema shunghuli za kiuchumi zimeongezeka sana pamoja na ongezeko la idadi ya Watu wenye uhitaji wa kuunganishiwa umeme nayo pi aim eongezeka kwa hivyo nitoe rai kwa mkandarasi kufanya kazi kwa kasi ili mradi huu ukamilike na wananchi wetu wapate umeme.” Alisisitiza Dkt. Kalemani wakati akihutubia kwenye hafla hiyo.
Alisema malengo ya serikali ni kuhakikisha wananchi wote mijini na vijijini wanapelekewa umeme ifikapo mwaka 2021/2022 ili waweze kunufaika kupitia huduma hiyo ya nishati katika kujiletea maendeleo.

No comments :

Post a Comment