GAVANA
wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Prof. Florens Luoga, (kushoto),
akimsikiliza Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika (Africa Group 1), Bi. Anne
Kabagambe, alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam Agosti 21,
2019.
GAVANA
wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Prof. Florens Luoga, (kushoto) na timu yake, akiwa kwenye mazungumzo na Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika (Africa Group 1), Bi. Anne
Kabagambe na timu yake ofisni kwa Gavana jijini Dar es Salaam. (PICHA NA INNOCENT MMARI WA BoT).
NA MWANDISHI WETU.
GAVANA
wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Prof. Florens Luoga, amekutana na Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya Dunia Kanda ya
Afrika (Africa Group 1), Bi. Anne Kabagambe, ofisini kwake jijini Dar es Salaam Agosti 21, 2019.
Afrika (Africa Group 1), Bi. Anne Kabagambe, ofisini kwake jijini Dar es Salaam Agosti 21, 2019.
Gavana
Luoga amemweleza Bi. Kabagambe hatua mbalimbali ambazo BoT inachukua
kuhakikisha kuna ukuaji wa uchumi, kuimarisha sekta ya mabenki, mifumo ya
malipo na huduma jumuishi za kifedha.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia aliipongeza BoT kwa hatua
mbalimbali inazochukua kutekeleza sera ya fedha na kueleza utayari wa Benki ya
Dunia kushirikiana katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo.
Katika
mazungumzo hayo pia Manaibu Gavana wa BoT, Dkt. Yamungu Kayandabila na Dkt.
Bernard Kibesse na Mshauri Mwandamizi wa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji huyo, Bw.
Zarau Kibwe, walihudhuria.
No comments :
Post a Comment