Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo
Agost 21,2019 amekutana na kuzungumza na Mratibu Mkazi wa Umoja wa
Mataifa Bw. Alvaro Rodriguez Wakati Bw. Alvaro alipofika Ofisini kwa
Makamu wa Rais Ikulu Jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kumuaga Makamu wa
Rais baada ya kumaliza kipindi chake cha Uwakilishi hapa Nchini
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa akutana na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa,anaye
maliza muda wake hapa Nchini Tanzania Bw. Alvaro Rodriguez .kwa ajili
ya kumuaga Waziri Mkuu ofisini kwake .Magogoni jijini Dar es Salaam.leo
Agosti 21.2019
UMOJA
wa Mataifa (UN) umeipongeza Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wake
Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna inavyotumia vizuri rasilimali
zake za ndani na hivyo kuiwezesha kutekeleza shughuli mbalimbali za
kimaendeleo sambamba na kupunguza utegemezi kutoka nje.
Pongezi
hizo zimetolewa leo (Jumatano, Agosti 21, 2019) na Mratibu Mkazi wa
Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez kwa nyakati tofauti wakati
alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu
Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa jijini Dar es Salaam.
Mratibu
huyo Mkazi wa Umoja wa Mataifa ambaye alikwenda kuagana na viongozi hao
baada ya kumaliza muda wake wa utumishi wa taasisi hiyo ya Kimataifa
hapa nchini alisema Tanzania imeendelea kutumia vizuri mapato yake ya
ndani kwa kuimarisha miundombinu na huduma za kijamii kama ujenzi wa
hospitali na vituo vya afya.
“Katika
kipindi changu cha miaka mitano ambacho nimefanya kazi Tanzania,
nimeshuhudia mabadiliko makubwa ya kimaendeleo yanayofanywa na Serikali,
ikiwemo kuimarika kwa mahusiano kati ya Serikali na Umoja wa Mataifa na
taasisi zake nchini.”
Katika
hatua nyingine, Bw. Rodriguez ameisifu Serikali ya Tanzania kwa namna
ilivyoweza kuandaa na kuendesha vizuri mkutano wa Wakuu wa Nchi na
Serikali za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika
Agosti 17 na 18 mwaka huu.
Mbali
na kuisifu Serikali pia kiongozi huyo amevipongeza vyombo vya habari
kwa jinsi vilivyoshirikiana na Serikali kuripoti matukio mbalimbali ya
mkutano huo. “Nawapongeza na wananchi kwa ushirikiano walioutoa kwa
Serikali wakati wote wa mkutano wa SADC.”





No comments :
Post a Comment