Waziri wa Maliasili na
Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akifungua Maonesho ya Wajenzi mwaka 2019 jijini
Dodoma leo, maonesho hayo yamehusisha makampuni yanayojishughulisha na ujenzi
zaidi ya 50. Kushoto kwake ni Mkuu wa wilaya ya Dodoma Mhe. Patrobas
Katambi na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Bw. Godwin Kunambi.
Waziri wa Maliasili na
Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akipata maelezo kuhusu bidhaa na huduma
zinazotolewa na makampuni ya ujenzi wakati wa Maonesho ya Wajenzi kwa
mwaka 2019 jijini Dodoma.
Waziri wa Maliasili na
Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akisoma maelezo ya huduma alipotembelea banda
la maonesho la Kampuni ya Mwanza Plastic Limited (MPL) wazalishaji na
wasambazaji wa bidhaa za plastiki yakiwemo mabomba ya maji wakati wa maonesho
ya Wajenzi kwa mwaka 2019 jijini Dodoma leo.
Waziri wa Maliasili na
Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiangalia vifaa vya umeme vinavyozalishwa na
makampuni ya Tanzania wakati wa maonesho ya Wajenzi ya mwaka 2019 jijini Dodoma
leo.
Waziri wa Maliasili na
Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akipata maelezo kuhusu bidhaa za rangi kutoka
kampuni ya Jotun mara baada ya kufungua Maonesho ya Wajenzi kwa mwaka 2019
jijini Dodoma leo.
Waziri wa Maliasili na
Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa
Maonesho ya Wajenzi kwa mwaka 2019 jijini Dodoma leo.
No comments :
Post a Comment