NA EMMANUEL MBATILO
Taasisi ya Chakula na
lishe imewataka watu waishio mijini waweze kuboresha lishe zao ili
waweze kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza.
Akizungumza na
wanahabari jijini Dar es Salaam, mkurugenzi wa idara ya elimu na mafunzo
ya lishe kutoka taasisi ya Lishe Bi. Sikitu Kihinga amesema kuwa
ukiangalia data ambazo
zipo kwasasa inaonyesha kwamba ishu ya uzito
uliozidi iko kubwa katika mijini ukilinganisha na sehemu ya mijini.
“Tumekutana hapa ili
tuweze kuangalia ni mikakati gani tunaweza kufanya kwa pamoja ili
kuhakikisha kwamba Lishe yetu inaimarika katika maeneo ya mijini”.
Amesema Bi. Sikitu.
Aidha Bi. Sikitu
ameongeza kuwa mtindo wa maisha tulionao kama vile kula vyakula vyenye
mafuta yaliyozidi na kutokufanya mazoezi kusababisha kuzidi kwa uzito na
magonjwa mbalimbali yasiyoambukiza.
“Watu wanaolisha watu
mijini (Mama Lishe) kuna vitu mbalimbali ambavyo tunaweza kuwasaidia
kwasababu tunaona watu wengi wanaoishi mijini huwa hawana muda wa
kuandaa vyakula hivyo kuwalazimu kwenda kwa mamalishe”. Ameongeza Bi.
Sikitu.
Pamoja na hayo Bi.
Sikitu amesema kuwa kukaa na mama Lishe waweze kuona ni mikakati gani
wanaweza kufanya na kuwasaidia ili kwamba wanahakikisha wanafanya Lishe
kwa watu wanaoishi mijini kuwa vizuri.
Kwa upande wa Afisa
mipango wa Shirika la Global alience for improve Nutrition, Dkt.
Winfrida Maila amesema kuwa wanatakiwa kuweka mazingira mazuri kwa mama
Lishe ili kuweza kuwashawishi watu wengi kupata chakula katika maeneo
hayo.
“Chakula kinatakiwa kuwa
katika makundi matano muhimu na si tu wanga kuwa mwingi, wanatakiwa
watumie vyakula mchanganyiko”. Amesema Dkt. Winfrida
No comments :
Post a Comment