Thursday, May 9, 2019

WAJASIRIAMALI WADOGO WAIOMBA SERIKALI KUWATAFUTIA MUWEKEZAJI ATAKAYE FUNGUA KIWANDA CHA VIFUNGASHIO

https://www.directory.co.tz/business?q=Mikopo+ya+wajasiriamali+
IMG_20190508_121901
Na Woinde Shizza, Arusha
Wajasiriamali wadogo wameiomba serikali kuwatafutia muwekezaji atakaewaletea mashine za
kutengeneza vifungashio pamoja na lebo ilikuweza kupunguza usumbufu wanaoupata. 
Iwapo tutapata vifungashio  bora na vizuri hitasaidia kukuza biashara yetu na kufanya bidhaa zetu kuwa juu zenye ubora kitaifa na kimataifa zaidi. 
Hayo yamebainishwa Leo na mjasiriamali Annet Kivuyo alipokuwa akiongea Katika semina ya wajasiriamali iliandaliwa na shirika la uthibiti wa Viwango(TBS) kwa kushirokiana na Sido ambapo alisema kuwa changamoto ya vifungashio inachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza soko la bidhaa za hapa nchini kwa sababu vifungashio vyetu avipo kwenye ubora unao kubalika. 
“vifungashio bora vyakuvutia vitasaidia bidhaa zetu ziwe kwenye viwango vyenye ubora , serikali itushulikie tuwe na mtu atakae wekeza mashine za lebo na kutengeneza vifungashio kama wenzetu wa nchi jirani kwani kwa sasa tunaagiza nchi za nje na vinavyokuja pia vinakuwa vichache avitoshelezi mahitaji “alisema annet
Alisema Tanzania  tunabidhaa nzuri na vyenye ubora ila shida kubwa inayotusumbua ni vifungashio hivyo aliitaji serikali ijitaidi kupata muekezaji atakae saidia kuondoa tatizo Hili.  
Kwa upande wake mkurugenzi wa TBS Jabir Abdi alisema kuwa wameamua kufanya mafunzo haya kwa wafanyabiashara wachakataji  wa bidhaa za ngozi  lakini pia huu ni muendelezo wa kuhakikisha wanapata elimu sahihi itakayo wasaidia kufikia viwango vya kitaifa  ili waweze kuuza bidhaa zao sio tu hapa nchini  pia waweze kuuza nje ya nchi
Aidha alifafanua kuwa wanatoa elimu hii pia ili waweze kupata alama za ubora pamoja na kuwawezesha kufikia malengo yao, kitu pekee kitakachowawezesha wajasiriamali kufikia malengo ni kufata sheria ya kufika viwango vya kitaifa.

No comments :

Post a Comment