Saturday, April 27, 2019

SPIKA NDUGAI AFUNGUA WARSHA YA UFUATILIAJI NA TATHMINI ZA SERA NA PROGRAMU ZA MAENDELEO BUNGENI JIJINI DODOMA


V25A3630A
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Wabunge na Wajumbe Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania na wawezeshaji kutoka nchi za Uganda na Srilanka(hawapo kwenye picha) wakati akifungua warsha ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Sera na Programu za Maendeleo kikao kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. Kulia ni Mwenyekiti Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania (TanEA), Dkt. Francis Mwijande, Katibu wa Wabunge Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania , Dkt. Semesi Sware (wa pili kushoto) na Mjumbe kutoka Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania (TanEA), Ndg. Isaac Kiwango
V25A3557A
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Wabunge na Wajumbe Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania (TanEA) pamoja na wawezeshaji kutoka nchi za Uganda na Srilanka wakati akifungua warsha ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Sera na Programu za Maendeleo kikao kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
V25A3513A
Katibu wa Wabunge wa Afrika upande wa Tanzania Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania (wa pili kushoto), Dkt. Semesi Sware akizungumza na Wabunge Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania(hawapo kwenye picha) na wawezeshaji kutoka nchi za Uganda na Srilanka wakati akifungua warsha ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Sera na Programu za Maendeleo kikao kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. Wa pili kulia ni Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai, Mwenyekiti Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania (TanEA), Dkt. Francis Mwijande (wa pili kulia) na Mjumbe kutoka Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania (TanEA), Ndg. Isaac Kiwango
V25A3592A
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia warsha iliyotolewa na Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania (TanEA) kikao kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
V25A3704A
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania na wawezeshaji kutoka Uganda na Srilanka baada ya kufungua warsha ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Sera na Programu za Maendeleo tukio lililofanyika leo nje ya Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
V25A3672A
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Wabunge, Wajumbe Chama cha Tathmini na Ufuatiliaji Tanzania na Wawezeshaji kutoka nchi za Uganda na Srilanka baada ya kufungua warsha ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Sera na Programu za Maendeleo tukio lililofanyika leo nje ya Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments :

Post a Comment