Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa
akipokelewa na Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai kabla ya kuanza kwa mechi
ya mpira wa miguu kati ya timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyochezwa leo katika Uwanja
wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mwenye Kijani ni Spika wa Baraza la
Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Zubeir Ali Maulid, Mbunge Viti Maalum, Mhe.
Salma Kikwete (wa pili kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Pastobas
Katambi (katikati). Mechi hiyo iliisha kwa timu zote mbili kufunga
magoli 2 -2, Lengo likiwa ni kuboresha uhusiano baina ya Mabunge hayo
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai
akiteta jambo na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kabla ya kuanza
kwa mechi ya mpira wa miguu kati ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyochezwa leo katika Uwanja
wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mechi hiyo iliisha kwa timu zote mbili
kufunga magoli 2 -2, Lengo likiwa ni kuboresha uhusiano baina ya Mabunge
hayo
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa
(kulia), Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia) wakifuatilia
mechi kati ya timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Baraza
la Wawakilishi Zanzibar iliyochezwa leo katika Uwanja wa Jamhuri Jijini
Dodoma. Watatu kushoto ni Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar, Mhe.
Shamsi Vuai Nahodha na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Pastobas Katambi
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania wakishangilia goli walilofunga dhidi ya Baraza la
Wawakilishi Zanzibar mchezo uliochezwa leo katika Uwanja wa Jamhuri
Jijini Dodoma. Kuanzia kushoto ni Mbunge wa Iringa Mjini, Mhe. Mch.
Peter Msigwa, Mbunge wa Mafinga Mjini Mhe. Cosato Chumi na Mbunge wa
Kilolo Mhe. Venance Mwamoto ambaye pia ni mfungaji wa goli hilo na nyuma
ni Ndg. Onesmo lau lau. Katika mchezo huo timu hizo zilifungana magoli 2
-2, Lengo likiwa ni kuboresha uhusiano baina ya Mabunge hayo
Wachezaji wa timu ya Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (kulia) wakisalimiana na Wachezaji wa
timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kabla ya kuanza kwa mechi ya
kirafiki baina yao iliyochezwa katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Mechi hiyo iliisha kwa timu hizo kufungana magoli 2 -2, Lengo likiwa ni
kuboresha uhusiano baina ya Mabunge hayo
Mbunge wa Kilolo, Mhe. Venance
Mwamoto (katikati) ambae pia ni Kocha Mchezaji na Mfungaji wa bao la
kwanza la timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akizungumza
na Wachezaji wa timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati
wa mapumziko katika mechi iliyowakutanisha timu hiyo na timu ya Baraza
la Wawakilishi Zanzibar iliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuri Jijini
Dodoma. Mechi hiyo iliisha kwa timu hizo kufungana magoli 2 -2, Lengo
likiwa ni kuboresha uhusiano baina ya Mabunge hayo
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)
No comments :
Post a Comment