Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James akimkabidhi Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati,
Dkt. Hamisi Mwinyimvua, hundi kifani ya dola milioni 309.65 (sh. bilioni
688.65), ambazo ni malipo ya awali (Advance Payment) kwa Mkandarasi
Kampuni ya Misri, inayojenga Mradi wa kuzalisha umeme wa Maporomoko ya
maji ya Mto Rufiji, mkoani Pwani, Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati,
Dkt. Hamisi Mwinyimvua, akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
wa Shirika la Umeme la Tanzania-TANESCO, Dkt. Alexender Kyaruzi, hundi
kifani ya dola milioni 309.65 (sh. bilioni 688.65), ambazo ni malipo ya
awali (Advance Payment) kwa Mkandarasi Kampuni ya Misri, inayojenga
Mradi wa kuzalisha umeme wa Maporomoko ya Maji ya Mto Rufiji, mkoani
Pwani, Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
wa Shirika la Umeme la Tanzania-TANESCO, Dkt. Alexender Kyaruzi, (wa
pili kulia) akimkabidhi Naibu Mkurugenzi wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa
Maji wa Rufiji kwa niaba ya Mkandarasi Mhandisi Mohamed Hassan, hundi
kifani ya dola milioni 309.65 (sh. bilioni 688.65), ambazo ni malipo ya
awali (Advance Payment) kwa Mkandarasi Kampuni ya Misri, inayojenga
Mradi wa kuzalisha umeme wa Maporomoko ya Maji ya Mto Rufiji, mkoani
Pwani, Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James, (katikati) akiongea na wanahabari (hawapo
pichani) kabla ya kukabidhi hundi kifani ya dola milioni 309.65 (sh.
bilioni 688.65) kwa niaba ya Serikali, ambazo ni malipo ya awali
(Advance Payment) kwa Mkandarasi Kampuni ya Misri, inayojenga Mradi wa
kuzalisha umeme wa Maporomoko ya maji ya Mto Rufiji, mkoani Pwani,
Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James, akiagana na Mkandarasi ambaye ni Naibu
Mkurugenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme wa maji wa Mto Rufiji Mhandisi
Mohamed Hassan, baada ya kukabidhiwa hundi kifani ya dola milioni 309.65
(sh. bilioni 688.65), ambazo ni malipo ya awali (Advance Payment) kwa
ajili ya kuanza rasmi kwa ujenzi wa mradi huo. tukio hilo limefanyika
Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Eva Valerian-Wizara ya Fedha na Mipang
………………………………………………………………………………………………
Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
Ni tukio la kihistoria ambapo
leo, Aprili 24, 2019, Serikali ya Tanzania, imetoa dola za Marekani
milioni 309.65, sawa na takriban shilingi bilioni 688.65, fedha zake za
ndani, kama
malipo ya awali kwa Mkandarasi – Arab Contractors ya Misri,
wanaojenga mradi wa kuzalisha umeme unaotokana na maporomoko ya maji ya
Mto Rufiji, mkoani Pwani.
“Haijapata kutokea katika
historia ya nchi hii Serikali kutoa fedha nyingi za malipo ya awali ya
kiasi kama hiki cha shilingi bilioni 688.65 katika mradi wa aina yoyote
uliowahi kutekelezwa hapa nchini isipokuwa huu” alisema Bw. Doto James,
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango.
Bw, Doto James, ambaye pia ndiye
Mlipaji Mkuu wa Serikali, alimkabidhi hundi kifani ya dola za Marekani
milioni 309.65, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua,
ambaye alimkabidhi hundi hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya
Shirika la Ugavi wa Umeme nchini-TANESCO, Dkt. Alexender Kyaruzi, ambaye
pia alimkabidhi hundi hiyo Naibu Mkurugenzi wa Ujenzi wa mradi huo
Mhandisi Mohamed Hassan, kwa niaba ya kampuni za Arab Contractors (Osman
A. Osman & Co na Elsewedy Electric S.A.E (AC-EE JV).
Alisema kuwa kiasi kilichotolewa
cha shilingi bilioni 688.65 ni sawa na asilimia 70 ya zaidi ya shilingi
trilioni 1 ya malipo ya awali yanayotakiwa kutolewa ya asilimia 15 ya
mradi huo ambao hadi kukamilika kwake ndani ya miaka mitatu ijayo,
unakadiriwa utagharimu zaidi ya shilingi trilioni 6.6.
Bw. James amezitaja baadhi ya
faida za mradi huo utakapo kamilika na kuzalisha megawati 2,115 za umeme
kuwa ni pamoja na nchi kuwa na umeme wa kutosha na wa uhakika,
kuongezeka kwa uwekezaji katika sekta ya viwanda vitakavyo chochea
uzalishaji wa bidhaa, ajira pamoja na upatikanaji wa maji ya uhakika
katika maeneo yanayozunguka mradi na mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
“Ninamtaka Mkandarasi akamilishe
mradi huu kwa wakati na kama ilivyokubaliwa kwenye mkataba ili mradi
utakapo kamilika uwe kichocheo muhimu cha kuiwezesha Tanzania kufikia
azma yake ya kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025” alisisitiza Bw.
Doto James
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati Dkt. Hamisi Mwinyimvua, alifafanua kuwa kwa mujibu wa
kifungu Na. 14.2 cha Mkataba, malipo ya awali ya Mkandarasi ni asilimia
15 ambazo zimegawanywa katika sehemu mbili ambapo asilimia 70 zinalipwa
kwa kutumia sarafu ya kigeni (dola za Marekani 309.645m) na asilimia 30
zitalipwa kwa fedha za ndani ambazo zitalipwa baada ya Mkandarasi
kukamilisha taratibu za kimkataba zinazohusu malipo hayo.
“Ninao uhakika kwamba malipo haya
ya awali yatamwezesha Mkandarasi kukamilisha taratibu za kupeleka vifaa
katika eneo la mradi na kuanza ujenzi mara moja kwa mujibu wa Mkataba.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi ya TANESCO, Dkt. Alexender Kyaruzi, alisema uzalishaji wa
umeme hapa nchini umefikia megawati 1600 na kwamba kuongezeka kwa
megawati nyingine 2,115 ni hatua kubwa na ya furaha na amemshukuru
Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kutekeleza
mradi huo.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa
Mkandarasi wa mradi huo Mhandisi Mohamed Hassan ameishukuru Serikali na
wananchi kwa ushirikiano mkubwa wanaoupata na amewahakikishia watanzania
kwamba mradi huo utatekelezwa kwa haraka na kwa viwango ili kutimiza
matarajio ya nchi ambayo ni maendeleo.
No comments :
Post a Comment