KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa
Magharib wakikagua mradi wa Maji Safi na Salama uliotekelezwa chini
Mfuko wa Jimbo la Kiembe Samaki katika ziara yao ya kukagua utekelezaji
wa Ilani ya CCM.
DIWANI wa Wadi ya Mbweni Unguja
Ndugu Maabadi Ali Maulid akitoa maelezo juu ya usambazaji wa mipira ya
maji Safi na Salama katika maeneo mbali mbali ya Wadi hiyo.
………………………………………………………………………………………
NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa
wa Magharibi Unguja kimewataka viongozi wa Jimbo la Kiembe Samaki
kuongeza kasi ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ili kutatua changamoto
zinazowakabili Wananchi.
Rai hiyo imetolewa na
Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huo Ndugu Mohamed Rajab Soud katika mwendelezo
wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Mkoa ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya
CCM katika Jimbo la Kiembe Samaki.
Alisema pamoja na kutekelezwa
kwa miradi mbali mbali ya maendeleo kupitia fedha za mifuko ya maendeleo
ya Jimbo hilo bado kupanahitajika juhudi za ziara za kutatua kero za
wananchi katika sekta za Afya,Maji Safi na Salama pamoja na miondombinu
ya barabara za ndani.
Alisema lengo la ziara hiyo ni
kukagua miradi inayotekelezwa na viongozi hao kama thamani ya fedha
zinazoandikwa katika ripoti ya maendeleo ya Jimbo zinaendana na fedha
iliyotumika.
Aliwambia viongozi hao kuwa wahakikishe miradi wanayoitekeleza isaidie jamii husika badala ya watu wachache.
Aidha amewasihi Wananchi wa
Jimbo hilo kuithamini na kuitunza miradi mbali inayotekelezwa kupitia
Ilani ya CCM ili iwanufaishe vizazi vya sasa na vijavyo.
“Utekelezaji wa Ilani ya CCM
ndani ya Jimbo la Kiembe Samaki unafanuyika lakini bado sijaridhika kwa
baadhi ya maeneo hivyo wahusika wanatakiwa kuongeza kasi kubwa katika
kutatua kero za wananchi.”,alieleza Mwenyekiti huyo Mohamed.
Naye Diwani wa Wadi ya Mbweni
Ndugu Maabadi Ali Maulid amesema katika kutatua kero za wananchi
wamejipanga kutekeleza miradi mikubwa mitatu ikiwemo kutengeneza minara
mitatu katika visima vya maji ili wananchi wapate huduma hiyo kwa
wakati.
Naye Afisa Mipango Manispaa ya Magharib ‘B’ Ndugu Saumu
Daniel Yussuf akizungumza katika Kituo cha Afya cha Kiembe Samaki
alisema wanaendelea kuimarisha huduma za Afya katika Vituo mbali mbali
licha ya kukabiliwa na changamoto za uchakavu wa majengo waliokabidhiwa
katika mfumo wa ugatuzi.
NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Magharibi Unguja
kimewataka viongozi wa Jimbo la Kiembe Samaki kuongeza kasi ya
utekelezaji wa Ilani ya CCM ili kutatua changamoto zinazowakabili
Wananchi.
Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huo Ndugu
Mohamed Rajab Soud katika mwendelezo wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Mkoa
ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Jimbo la Kiembe Samaki.
Alisema pamoja na kutekelezwa kwa miradi mbali mbali ya
maendeleo kupitia fedha za mifuko ya maendeleo ya Jimbo hilo bado
kupanahitajika juhudi za ziara za kutatua kero za wananchi katika sekta
za Afya,Maji Safi na Salama pamoja na miondombinu ya barabara za ndani.
Alisema lengo la ziara hiyo ni kukagua miradi
inayotekelezwa na viongozi hao kama thamani ya fedha zinazoandikwa
katika ripoti ya maendeleo ya Jimbo zinaendana na fedha iliyotumika.
Aliwambia viongozi hao kuwa wahakikishe miradi wanayoitekeleza isaidie jamii husika badala ya watu wachache.
Aidha amewasihi Wananchi wa Jimbo hilo kuithamini na
kuitunza miradi mbali inayotekelezwa kupitia Ilani ya CCM ili
iwanufaishe vizazi vya sasa na vijavyo.
“Utekelezaji wa Ilani ya CCM ndani ya Jimbo la Kiembe
Samaki unafanuyika lakini bado sijaridhika kwa baadhi ya maeneo hivyo
wahusika wanatakiwa kuongeza kasi kubwa katika kutatua kero za
wananchi.”,alieleza Mwenyekiti huyo Mohamed.
Naye Diwani wa Wadi ya Mbweni Ndugu Maabadi Ali Maulid
amesema katika kutatua kero za wananchi wamejipanga kutekeleza miradi
mikubwa mitatu ikiwemo kutengeneza minara mitatu katika visima vya maji
ili wananchi wapate huduma hiyo kwa wakati.
Naye Afisa Mipango Manispaa ya Magharib ‘B’ Ndugu Saumu
Daniel Yussuf akizungumza katika Kituo cha Afya cha Kiembe Samaki
alisema wanaendelea kuimarisha huduma za Afya katika Vituo mbali mbali
licha ya kukabiliwa na changamoto za uchakavu wa majengo waliokabidhiwa
katika mfumo wa ugatuzi.
No comments :
Post a Comment