Mkuu wa Mawasiliano wa Shirika la ndege la (ATCL) Bw Josephat Kigirwa.
……………………………………………………………………………
Ndege ya Shirika la Ndege la Air
Tanzania (ATCL) Boeing 787-8 Dreamlinner inatarajia kuanza safari zake
za nje ifikapo Julai mwaka huu, Akizungumza na waandishi wa habari
Mkuu wa Mawasiliano wa Shirika hilo Bw. Josephat Kigirwa amesema safari
hizo zitaaza tarehe 17 mwaka huu ambapo sambamba na safari za india
pia Juni 28 wataanza kutoa huduma kati ya usafiri wa Johnsburg Afika
Kusini na Dar es salaam safari zikiwa mara tatu kwa wiki.
Ameongeza kuwa huo ni mwendelezo
wa mpango wao mahsusi wa kupanua huduma za shirika hilo humu nchini na
nje ya nchi ambapo kwa sasa tayari wanatoa huduma katika mikoa 10 ya
Tanzania ikiwemo Kilimanjaro, Mbeya, Kagera, Kigoma, Mbeya, Mwanza,
Dodoma,Tabora, Shinyanga na Zanzibar, Kwa sasa tayari (ATCL) inatoa
huduma ya usafiri wa anga katika nchi 4 mpaka sasa ambazo ni Bujumbura
Burundi, Entebe Uganda, Lusaka Zambia na Harare Zimbabwe.
Josepaht Kigirwa ameongeza kuwa
kwa sasa wanafanya tafiti mbalimbali na matayarisho ili kuanzisha
safari zingine nchini ambapo wiki ijayo wataanza safari katika mkoa wa
Iringa na tayari wako katika utaratibu wa kujiweka sawa kwa ajili ya
kuongeza huduma katika Viwanja vya Mpanda Katavi, Mtwara mkoani Mtwara,
Songea Mkoani Ruvuma, Pemba Zanzibar na mkoa waTanga.
Waandishi wa habari wakimsikiliza Mkuu wa Mawasiliano wa Shirika la ndege la (ATCL) Bw Josephat Kigirwa.
No comments :
Post a Comment