Mkurugenzi mtendaji
wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini ( TPDC), Kapuulya Musomba,
(wa kwanza kulia) akieleza jambo. (picha na Mwamvua Mwinyi)
Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo
alipotembelea banda la Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (
TPDC),kwenye maonyesho ya bidhaa za viwandani huko Pichandege Kibaha
Pwani (picha na Mwamvua Mwinyi)
Msanii Afande Sele
alipotembelea banda la Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (
TPDC),kwenye maonyesho ya bidhaa za viwandani huko viwanja vya Sabasaba
Pichandege Kibaha Pwani (picha na Mwamvua Mwinyi)
……………………………………………………………..
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA
SHIRIKA la Maendeleo
ya Petroli nchini ( TPDC), linatarajia kuongeza vituo 10 hadi 20 kwa
Dar es salaam -Mtwara -Lindi, vya kujaza gesi asilia kwenye magari
yaliyowekewa mfumo huo ambapo kipo kituo kimoja Ubungo ,kwa miaka kumi
sasa ambacho hakikidhi mahitaji.
Ili
kufikia malengo yake ya kuongeza vituo vingi katika maeneo mbalimbali
limejipanga kuruhusu na kukubaliana na watu binafsi wenye vituo vya mafuta kuweka gesi kwenye vituo vyao .
limejipanga kuruhusu na kukubaliana na watu binafsi wenye vituo vya mafuta kuweka gesi kwenye vituo vyao .
Akitembelea maonyesho
ya bidhaa za viwandani yanayoendelea viwanja vya sabasaba, Pichandege
Kibaha Pwani, Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli
nchini ( TPDC), Kapuulya Musomba, alisema mwamko wa watumiaji upo
vizuri tatizo hakuna vituo mikoani.
Alieleza mwaka ujao wa fedha wataongeza vituo hivyo na sasa wapo kwenye hatua ya manunuzi.
Musomba alisema
,wataanza kuongeza vituo viwili ama vitatu Dar es salaam na kuendelea
maeneo mengine, na kusema watatangaza tenda ili wawekezaji na watu
binafsi wajitokeze kufanikisha hilo.
“Gesi asilia
ikitumika kwenye magari inaweza kupunguza zaidi ya nusu ya gharama
mafuta na kuleta unafuu katika sekta ya usafirishaji nchini,
“Wadau washirikiane nasi kwa kupata ufafanuzi EWURA na TPDC ili kufanya makubaliano “alisisitiza Musomba.
Hata hivyo alitaja
mpango mwingine ni kuona wananchi wanafaidika na raslimali ya gesi
lakini wanakwenda kwa awamu kulingana na fedha wanayoipata.
“Gesi kwa ajili ya
majumbani tumeanza Dar es salaam na Mtwara, na kuhusu viwandani
tumeshaanza Pwani, Dar es salaam na Mtwara kwa njia ya mabomba “
Musomba
alielezea,mwaka huu wa fedha kufikia 2019 watapeleka Kibaha kwa mitungi
kwa kuwa mabomba hayajafika kwa kujazia Dar es salaam kisha kuwafikishia
wananchi.
Alifafanua kwa wale
wa mikoa mingine wameshaanza utafiti wa kina kuona kama watoa bomba Dar
es salaam, Kibaha, Bagamoyo, Chalinze, Tanga litembee kwenye mikoa kama
nane na kwa kushirikiana na wadau watafikia lengo hilo.
Nae Mkuu wa mkoa wa
Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo alisema TPDC ni mdau mkubwa mkoani humo
kwani mkoa huo ni wa viwanda na baadhi ya wawekezaji wameanza kutumia
gesi kwa matumizi yao.
Alisema alieleza eneo
jingine ni wakati ujenzi wa bandari mpya Bagamoyo ukianza watahitaji
gesi kutokana na ujenzi kuambatana na viwanda vingi.
Ndikilo alibainisha
awamu ya kwanza ya ujenzi huo utaendana na ujenzi wa viwanda 190 ambapo
awamu ya pili utakuwa na takriban viwanda 1,000 hivyo gesi itahitajika
pia.
No comments :
Post a Comment