Thursday, October 11, 2018

SERIKALI YAWASHUKIA WALIOSHINDWA KUENDELEZA VIWANDA


20181010_105148

MTWARA
Na,Omary Hussein.
Naibu waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Stella Manyanya amewataka wawekezaji walioshindwa kuendeleza maeneo yao kwa muda mrefu, hususani wamiliki wa viwanda vilivyo binafsishwa, kutumia busara kwa kueleza ukweli ili serikali ichukue hatua ya kuviwezesha viwanda hivyo kufanya kazi.
20181010_115340
Naibu waziri ameyasema hayo Mkoani Mtwara akiwa katika kiwanda cha kutengeneza Cement cha  Dangote, baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku moja, iliyolenga kujiridhisha na hali ya viwanda mkoanihumo.
20181010_122923
‘Sisi kama serikali tusingependa kuona wawekezaji wakashindwa kujiendeleza bila sisi kuwasaidi lakini ni kwawale tu wenye nia ya dhati ya kuwekeza,niwahakikishie tu wawekezaji Tanzania ukiwemo mkoa huu wa mtwara nisehemu salama kwa wawekezaji wenye nia, nasisi tutakua nao bega wa bega’ alisema Naibu waziri Manyanya.
 20181010_130347
“Ila kwa wale ambao wanataka kujaribu kutuchezea wnasema wanawekeza lakini hawana nia ya kuwekeza pengine wanatafuta tu fursa za kushika soko ili waonekane wamezuia halafu wanawekeza maeneo mengine kwakweli hao hatutawavumulia” Aliongeza Naibu waziri Manyanya.
 20181010_131642
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mtwara Evod Mmanda ameshukuru ujio wa Naibu waziri huyo akisema wanapokuja viongozi wa juu inasaidi kuweka hamasha kwa wawekezaji wakiona serikali yao ipo pamojanao na inawaunga mkono kwa vitendo.
20181010_145112
“Ujio wa naibu waziri katika wilaya ya Mtwara sio wakazi wa Mtwara pekeyao wanao nufaika bali inasaidia hata kwa wawekezaji wanaoendesha viwanda pamoja na wafanyakazi kuona serikali inawajali”.Alisema mkuu wa wilaya ya Mtwara Evod Mmanda.

No comments :

Post a Comment