Wednesday, October 31, 2018

SERIKALI YAONYA WATUMISHI WAKE KUTOKUSHABIKIA VYAMA VYA SIASA


0
Kaimu Mkurugenzi wa idara ya Gharama za Uchaguzi na Misaada Bi. Piencia Kiure akifungua mafunzo ya siku mbili juu ya Sheria za Gharama za Uchaguzi na Maadili ya Vyama vya Siasa yanayoendelea  leo katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa jijini Dar es Salaam.
1
Msajili wa Vyama vya Siasa Mhe. Jaji Francis Mutungi (wa tatu kushoto)  akisisitiza jambo wakati wa majadiliano katika mafunzo ya siku mbili juu ya Sheria za Gharama za Uchaguzi na Maadili ya Vyama vya Siasa yaliyoanza  leo katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa jijini Dar es Salaam.
2
Bi. Esther Mwanri, Mratibu wa mafunzo akitoa mada kuhusu maana, lengo la Sheria ya Gharama za Uchaguzi na jinsi ya ujazazi wa fomu za Gharama za Uchaguzi.
3
Mmoja wa washiriki akichangia hoja wakati wa majadiliano
4 6
Baadhi ya washiriki wakifuatilia kwa makini wakati wa mafunzo
8
Msajili wa Vyama vya Siasa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mafunzo
………………………
Maafisa wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa wanaojiandaa kushiriki katika uangalizi wa kampeni za uchaguzi unaotegemea kufanyika Decemba 2 mwaka huu, wameaswa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sheria ili kujikita katika kuhudumia Vyama vyote kwa usawa.
Hayo yamesemwa leo na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Gharama za Uchaguzi na Misaada Bi. Piencia Kiure wakati akifungua mafunzo ya siku mbili juu ya Sheria za Gharama za
Uchaguzi na Maadili ya Vyama vya Siasa kwa niaba ya Msajili wa Vyama vya Siasa Mhe. Jaji Francis S. K Mutungi yanayoendelea kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia kuhusu mafunzo hayo, mratibu wa mafunzo, Bi. Esther Mwanri amesema kuwa mafunzo hayo ni muendelezo wa mafunzo ambayo hutolewa na ofisi hiyo kwa maafisa ambao hushiriki katika uangalizi wa chaguzi za Madiwani, Wabunge na Urais yakiwa na lengo la kuwakumbusha washiriki taratibu na sheria mbalimbali zinzzozimamiwa na Ofisi ya msajili wa Vyama vya Siasa na  zinazotakiwa kutekelezwa na wagombea na vyama vya siasa nyakati za chaguzi.
Bi. Mwanri amebainisha kuwa baadhi ya mada ambazo zimewasilishwa na zitakazowasilishwa ni pamoja na maana na lengo la Sheria ya Gharama za Uchaguzi, matendo yaliyokatazwa katika kampeni za uchaguzi, Fomu zinazohitajika kujazwa na wagombea na vyama vya siasa na namna ya kuzijaza. Elimu ya maadili ya vyama vya siasa, haki ya vyama vya siasa, wajibu wa Vyama vya Siasa na wajibu wa Msajili wa Vyama vya Siasa.
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ni taasisi iliyopo kwa mujibu wa kisheria ambayo ina wajibu wa kusimamia vyama vya siasa nchini ili viweze kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Gharama za Uchaguzi.

No comments :

Post a Comment