Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam
Mhe. Paul Makonda leo ameunda kamati ya watu 17 watakaofanya operesheni
kabambe ya kuwafundisha adabu watu wanaofanya ushoga, nyumba
zinazotumika kurekodi video za Ngono, wanaojiuza na matapeli wa njia ya
mitandao.
RC Makonda amesema kamati hiyo
inajumuisha maafisa wa Polis, TCRA, Wanasheria, Bodi ya Filamu,
Madaktari na Wataalamu wa ushauri na Saha ambapo kamati hiyo itaanza
zoezi la kamatakamata jumatatu.
Operesheni hiyo imepokelewa kwa
mikono miwili na mamilioni ya wananchi ambao wamekuwa wakichukizwa na
mmomonyoko wa maadili ambapo RC Makonda hadi sasa amepokea SMS zaidi ya
18,000 za watu wanaopongeza na kutaja majina ya watu wanaofanya matendo
maovu ikiwemo ushoga na biashara ya ngono.
Aidha RC Makonda amesema hadi
sasa amepokea majina zaidi ya 200 ya mashoga waliotajwa wakiwemo kina
James Delicious, Dida Mtamu,Abas,Aunt Miliki na kundi la Pachupachu.
Pamoja na hayo RC Makonda amesema
oparesheni hiyo pia itahusisha sehemu za Masaji ambazo baaadhi yake
zimekuwa zikijihusisha na biashara ya ngono.
Hata hivyo RC Makonda amesema
kuwa hata wanaume watakaotajwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi (wateja)
wa Mashoga watakamatwa na kuchukuliwa hatua Kali za kisheria kwa mujibu
wa Sheria.
Sanjari na hayo RC Makonda ametoa
angalizo kwa watu wenye picha na video za ngono kwenye simu zao kuwa
operesheni hii haitowaacha salama.
No comments :
Post a Comment