Mkuu wa Masoko, Mawasililiano na
Mahusiano wa Benki ya KCB, Christine Manyenye(kulia) akizungumza na
waandishi wa habari leo kwenye mkutano wa makabidhiano ya misaada
mbalimbali ikiwemo vitanda 10 magodoro 10, mashuka 20, vyenye thamani ya
shilling 6,017,000 katika wodi ya wananwake Hospitali ya Amana Ilala
Jijini Dar Es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya
Amana, Dr. Amim Kilomoni.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali Ya
Amana, Dr. Amim Kilomoni akizungumza na waandishi wa habari kwenye
mkutano wa makabidhiano ya misaada mbalimbali toka Benki ya KCB ikiwemo
vitanda 10 magodoro 10, mashuka 20, vyenye thamani ya shilling 6,017,000
kwa wodi ya wanawake katika Hospitali hiyo leo jijini Dar Es Salaam.
Mkuu wa Masoko, Mawasililiano na
Mahusiano wa Benki ya KCB, Christine Manyenye (kushoto) akimkabidhi
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dkt. Amim Kilomoni moja kati ya
Vitanda na Vifaa vingine vyenye thamani ya Tsh 6,017,00/= kwa wodi ya
wanawake Hospitali ya Amana, Dar Es Salaam
Wafanyakazi wa KCB na Wauguzi wa
Hospitali ya Amana wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya Benki ya
KCB kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya TSh .
6,017,000 kwa wodi ya wanawake leo kwenye Hospitali ya Amana Ilala, Dar
Es Salaam.
Baadhi ya waandishi waliohudhuria mkutano wa makabidhiano.
………………………………………………………………………………
Benki ya KCB Tanzania imekabidhi
msaada wenye thamani ya milioni 6 kwa wodi ya wanawake katika Hospitali
ya Rufaa ya Amana, Ilala jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati wa hafla
ya makabidhiano Mkuu wa Masoko, Mawasililiano na
Mahusiano wa benki
hiyo, Christine Manyenye alisema kuwa mchango huo upo ndani ya
vipaumbele vya benki katika uwekezaji jamii kwa ajili ya kusaidia jamii
zilizo na uhitaji.“Benki ya KCB Tanzania inadhamini uwajibikaji kwa jamii ambayo kwa kiwango kikubwa inalenga maeneo ya vipaumbele vya Afya, Elimu, Mazingira, Ujasiriamali na masuala ya ubinadamu”, Bi. Manyenye alisema na kubainisha kwamba tangu benki hiyo ilipofungua milango yake hapa Tanzania mwaka 1997, imekuwa ikijikita katika kuisadia jamii.
Benki ya KCB ilikabidhi misaada
mbalimbali ikiwemo vitanda 10 magodoro 10, mashuka 20, vyenye thamani ya
shilling 6,017,000 katika Hospitali hiyo. Mkurugenzi huyo alisema kuwa
upungufu wa vitanda, magodoro na masuka katika hospitali nyingi nchini
ni changamoto hasa katika wodi za akina mama na watoto Benki ya KCB
iliamua kutoa msaada huo ilikupunguza changamoto hizo.
Akitolea mfano wa michango
iliyotolewa na benki hiyo katika kupunguza viwango vya vifo vya kinamama
na watoto nchini, Manyenye alisema: “Kupitia miradi hiyo Benki ya KCB
Tanzania imeshazisaidia hospitali zaidi ya 15 kwa kuzipatia vifaa
tiba mbalimbali.”
Alizitaja hospitali hizo kuwa ni
Muhimbili, Mwananyamala, Ocean Road Cancer Institute, Buguruni, Sinza,
Amana, Temeke na Kituo cha Afya cha Njia (Dar es Salaam); Mt. Meru na
Ngarenaro (Arusha); KCMC, St. Thomas na Mawenzi (Moshi); SDA na
Makongoro (Mwanza); Hospitali ya Morogoro (Morogoro); Kivunge Cottage
na Kituo cha Huduma za Afya Kombeni (Zanzibar) na Hospitali
ya Mkuranga (Pwani).
Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali Ya Amana, Dr. Amim Kilomoni aliishukuru KCB Bank kwa msaada waliotoa kwani utasaidia kupunguza changamoto zilizokuwa zinawakabili, ikiwamo uhaba wa vitanda, magodoro na mashuka.
Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali Ya Amana, Dr. Amim Kilomoni aliishukuru KCB Bank kwa msaada waliotoa kwani utasaidia kupunguza changamoto zilizokuwa zinawakabili, ikiwamo uhaba wa vitanda, magodoro na mashuka.
No comments :
Post a Comment