Kaimu Katibu Mkuu wa ALAT
Bw.Abadallah Ngodu akizungumza na Viongozi pamoja na Waandishi wa
Habari (hawapo Pichani) wakati wa kutoa Taarifa ya Mkutano Mkuu
unaotarajiwa kufanyika Septemba 24 hadi 28 Jijini Dodoma
Mwenyekiti wa ALAT Taifa
Bw.Gulamhafeez Mukadamu akitoa Taarifa kwa Waandishi wa Habari kuhusiana
na Mkutano Mkuu wa ALAT Unaotarajiwa kufanyika Septemba 24 hadi 28
mwaka huu jijini Dodoma.
Bw. Nsolo Mlozi Meneja wa NMB
kanda ya Kati akizungumza na Waandishi wa habari baada ya Benki yao
kutoa Ufadhili wa Mkutano Mkuu wa ALAT Unaotarajia kufanyika Septemba 24
hadi 28 Jijini Dodoma
Bw.Nsolo Mlozi Meneja NMB Kanda ya
kati akikabidhi hundi ya milioni kumi kwa Mwenyekiti wa ALAT Taifa,
Gulamhafeez Mukadamu, fedha hizo ni kwa ajili ya kufanikisha mkutano huo
Unaotarajia kufanyika Septemba 24 hadi 28 jijini Dodoma
……………………………
Na.Alex Sonna wa Fullshangweblog,Dodoma
Jumuiya ya Tawala za Mitaa
Tanzania (ALAT) intarajia kufanya mkutano wake mkuu wa 35 Septemba 24
hadi 28 mwaka huu Jijini Dodoma na Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais
Dkt.John Pombe Magufuli.
Akizungumza na Waandishi wa habari
Mwenyekiti wa ALAT Taifa Gulamhafeez Mukadamu,amesema kuwa maandalizi
ya Mkutano huu yameshakamilika na utafanyika katika Ukumbi wa Mkutano wa
Jakaya Kikwete Jijini Hapa na kuonngeza kuwa Jumuiya ya Tawala ya Mitaa
Tanzania ni chombo wakilishi na sauti ya pamoja ya Mamlaka ya serikali
za mitaa inayounganisha halmashauri zote za majiji,Manispaa,Miji na
wilaya Tanzania bara.
Na pia ameeleza kuwa Jumuiya jiyo
Ilianzishwa mwaka 1984,Desemba 13 Mjini Dodoma baada ya kureshwa kwa
mfumo wa Serikali za Mitaa kwa Sheria Sura Na.288 ya Sheria ya nchini.
“Majukumu ya msingi ya Jumuiya kwa
mujibu wa katiba ni kuwakilisha haki maslahi ya serikali za mitaa
katika vyombo mbalimbali nchini na nje ya nchi, kushawishi mabadiliko ya
sera na sheria kwa lengo la kuwezesha utekelezaji mzuri wa dhana ya
kupeleka madaraka kwa wananchi”amesma Mukadamu
Aidha amesema kuwa Alat hutoa
huduma za kusaidia Mamlaka ya Serikali za Mita katika nyanja mbalimbali
kwa lengo la kuboresha ufanisi na Utekelezaji wa majukumu yao na kuwa
jukwaa la upashanaji wa habari na kubadilishana uzoefu katika utoaji wa
huduma kwa wananchi.
Jambo lingine ni kujadili taarifa
ya mwaka ya utekelezaji wa shughuli za Jumuiya,kupokea na kujadili
taarifa ya fedha ya jumuiya na kujadili na kupitisha makadirio ya mapato
na matumizi jumuiya kwa mwaka 2018 na 19.
Mkutano Mkuu wa Alat unatarajiwa
kuhudhuliwa na wenyekiti wa Halmashauri zote,Wakurugenzi wa Mamlaka za
Serikali za Mitaa na Wabunge mmoja kutoka kila Mkoa wa Tanzania bara na
kufanya idadi ya washiriki kuwa zaidi ya 500 na kutakuwa na waalikwa
kutoka nchi mbalimbali.
Hata hivyo ALAT imetoa wito kwa
mashirika na wadau mbalimbali kufadhili mkutano huo ikiwa ni pamoja na
sehemu ya kutangaza bidhaa zao kwa lengo la kufanikisha mkutano huo kwa
manufaa ya kuboresha Maisha ya watanzania.
Katika Kufanikisha Mkutano huo
Benki ya NMB imekabidhi Hundi ya shilingi Milioni 100 kama sehemu ya
faida inayopatikana kutoka benki hiyo nchi.
Bw.Nsolo Mlozi ambaye ni Meneja
NMB Kanda ya kati akikabidhi hundi ya milioni kumi kwa Mwenyekiti wa
ALAT Taifa, Gulamhafeez Mukadamu,Mlozi alisema fedha hiyo ni kwa ajili
ya kufanikisha mkutano huo wa ALAT.
Mlozi amaesema kuwa NMB inatambua
mchango mkubwa ambazo hutolewa na halmashauri katika kufanikisha
shughuli za maendeleo na katika harakati za kuhakikisha halmashauri
zinafanikisha katika ukusanyaji wa mapato NMB kwa sasa imeweza
kuunganisha halmashauri 160 katika mfumo wa Elekroniki kwa ukusanyaji wa
mapato kwa kutumia mashine za Elekroniki.
Katika Mkutano Mkuu wa ALAT Wadau
pamoja na Viongozi wa Serikali wanatarajia kujadili mambo mbalimbali
ikiwa ni kuona ni namna gani ya kuishauri Serikali juu ya urudishwaji
wa vyanzo vya mapato vilivyochukuliwa na Serikali Kuu na kuzifanya
halmashauri kuwa na hali mbaya ya kiuchumi.
Aidha halimashauri nyingi
zimekuwa na uchumi kiduchu unatokana na serikali kuchukua vyanzo vingi
vya mapata na kuviingiza katika serikali kuu jambo ambalo lilioneonekana
kuwa kikwazo cha maendeleo katika halimashauri nyingi kwa kushindwa
kuwa na vyanzo vya mapato vya kutosha kama ilivyokuwa hapo awali.
No comments :
Post a Comment