Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya akitoa ufafaunizi hivi karibuni wakati warsha ya utetezi wa
majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji
iliyowahusisha viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani hapa.
NA
TIGANYA VINCENT-RS TABORA
MAAFISA Biashara Mkoani Tabora wametakiwa
kujitahidi kuwatembelea wafanyabiashara na kutoa elimu ambayo itawasaidia
kutambua wajibu wao wa kulipa kodi mbalimbali kwa hiari ili kuboresha makusanyo
ya mapato ya Serikali kwa ajili ya maendeleo ya Nchi.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Meneja
wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Ingembensabo Emmanuel Malunde wakati akifunga
warsha ya utetezi majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na
uwekezaji iliyowahusisha viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani hapa.
Alisema kuwa baadhi ya Maafisa hao wamekuwa
wakijikita katika kukusanya mapato bila kutoa elimu kwa wadau wao juu ya
uendeshaji wa biashara kwa tija na umuhimu wa wao kulipa kodi na ushuru wa
Serikali kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Malunde alisema ukosefu wa elimu wakati
mwingine ndio umekuwa ukisababisha wafanyabiashara kuvutana na Watendaji wa
umma wa sekta ya biashara bila sababu za msingi.
Alisema elimu ya kutosha itawezesha kujenga
urafiki kati yao na watendaji wa umma na hivyo kufanya mazingira ya ukusanyaji
kodi kuwa rahisi na kuondoa dhana ya baadhi ya kuona kama wananyanyaswa
na Maafisa Biashara.
Mmoja wa washiriki wa warsha hiyo Mhasibu Mkuu (CA) wa Chama Kikuu cha Ushirika wa
Tumbaku Kanda ya Magharibi(WETCU) Goodluck Amos alisema Maafisa Biashara ni
lazima watambue kuwa kila wakati kunatokea mabadiliko katika teknolojia na
uboreshaji wa mifumo ya ukusanyaji mapato ambayo pia wafanyabiashara wanapaswa
kuelimishwa kila wakati kunapokuwepo na mabadiliko.
Alisema hatua hiyo itawasaidia wao kwenda na
wakati na kuachana na mtindo wa kizamani wa kulipa mapato ya Serikali kwa ajili
ya kuwa na mazingira ambayo ni rafiki ya ulipaji wa kodi za Serikali.
Amos alisema wasipatiwa elimu ya kutosha baadhi
yao wanaweza kuendelea na mtindo wa kufanyabiashara ambayo haina tija kwao na
Serikali.
Warsha hiyo ya siku mbili iliandaliwa na Taasisi
ya Wafanyabiashara , Viwanda na Kilimo(TCCIA) Mkoa wa Tabora kwa kushirikiana
na Chuo Kikuu cha Dar es salaam shule ya Biashara kwa lengo kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji
kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani hapa.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua Haruna Kasela akitoa
maelezo kwa niaba yahivi karibuni wakati warsha ya utetezi wa majadiliano
katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji iliyowahusisha viongozi wa
Serikali na sekta binafsi mkoani hapa.
Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Ingembensabo Emmanuel
Malunde akifunga hivi karubuni warsha ya utetezi majadiliano katika
kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji iliyowahusisha viongozi wa
Serikali na sekta binafsi mkoani hapa.
No comments :
Post a Comment