Sunday, September 23, 2018

MAAFA YA MV NERERE: MATUKIO YA PICHA WAKATI WA MAZISHI LEO SEPTEMBE 23, 2018

 Askari wakiweka kaburibi miili ya baadhi ya  wananchi walifariki dunia katika ajali ya Kivuko cha MV Nyerere kilichozama kwenye  kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe wakati wa   mazishi yaliyoongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kijiji cha Bwisa kisiwani Bukara, Septemba 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka shada la maua kwenye kaburi  la mmoja wa wananchi walifariki katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere kilichozama katika katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. Majaliwa aliwaongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi yaliyofanyika kwenye kijiji hicho Septemba 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Wafanyakazi wa kujitolea na wakiungana na askari, wakiweka udongo wakati wa mazishi ya watu waliofariki kwenye ajali ya kivuko cha Mv Nyerere, pembezoni mwa ziwa Victoria huko Ukara, Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza leo Septemba 23, 2018. (PICHA NA MICKY JAGGER WA K-VIS BLOG)
 Wafanyakazi wa Msalaba Mwekundu na askari wa ulinzi na usalama, wakishusha majeneza yenye miili ya watu waliofariki kwenye ajali ya kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere, wakati wa mazishi yaliyofanyika pembezoni mwa Ziwa Victoria huko Ukara, Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza leo Septemba 23, 2018. 9PICHA NA MICKY JAGGER WA K-VIS BLOG)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimia na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama  wakati alipowasili katika kijiji cha Bwasa kwenye  kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe kushiriki katika mazishi ya wananchi waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere, Septemba 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa heshima kwenye kaburi  la mmoja wa wananchi walifariki katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere kilichozama   katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. Majaliwa aliwaongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi yaliyofanyika kwenye kijiji hicho Septemba 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapa pole wafiwa katika mazishi ya mwananchi waliofariki katika ajali ya Kivuko cha MV Nyerere kilichozama  katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. Majaliwa aliwaongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi yaliyofanyika kwenye kijiji cha Bwisa  kisiwani Ukara Septemba 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Ilemela, Angelina Mabula na viongozi wengine walioshiriki katika mazishi ya  baadhi ya wananchi waliofariki dunia katika ajali ya meli ya MV Nyerere katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe Septemba 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Ndugu wakiwa na huzuni wakati wa mazishi hayo. (PICHA NA K-VIS BLOG/MICKY JAGGER)
 Askari wakiandaa majeneza yenye miili ya watu waliofariki kwenye ajali yab kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere tarayari kwa mazishi leo Septemba 23, 2018. (PICHA NA K-VIS BLOG/MICKY JAGGER)
  Ndugu wakiwa na huzuni wakati wa mazishi hayo. (PICHA NA K-VIS BLOG/MICKY JAGGER)
 Ndugu wa marehemu wakiwa na mashada ya maua wakati wa mazishi ya wapendwa wao leo Septemba 23, 2018. 9PICHA NA K-VIS BLOG/MICKY JAGGER)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohammed Abood  (wapili kulia) akiungana na Masheikh katika  sala kwenye mazishi ya wananchi waliofariki dunia katika ajali ya Kivuko cha MV Nyerere kilichozama katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. Mazishi hayo yaliongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kijiji cha Bwisa  kisiwani Bukara, Septemba 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Askofu wa Jimbo Katoliki la Bunda, Renatus Nkwande akiomba katika  mazishi ya wananchi waliofariki dunia katika ajali ya Kivuko cha MV  Nyerere kilichozama katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. Mazishi hayo yaliyoongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa yalifanyika katika kijiji cha Bwisa kisiwani Bukara, Septemba  23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza kwenye mazishi hayo. (PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipewa maelezo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella kuhusu juhudi zinazofanywa  na wahandishi za kukivuta kivuko cha MV Nyerere kilichozama katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe wakati aliposhiriki katika mazishi ya wananchi waliokufa katika ajali ya kivuko hicho kwenye kijiji cha Bwisa kisiwani Ukara Septemba 23, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mv Nyerere, akiwa amelala kifudifudi huku akiacha Zaidi ya watu 225 wakipoteza Maisha. Juhudi za kukipindua kivuko hicho zimeanza ikli kuona kama kuna miili Zaidi. 9PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

No comments :

Post a Comment