Thursday, September 27, 2018

CHUO KIKUU MZUMBE CHAPONGEZWA KWA KONGAMANO LA TATHMINI NA UFUATILIAJI


1 (4)
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  ( TAMISEMI) Dkt. Zainab Chaula akisisitiza jambo wakati wa hafla ya kufunga  Kongamano la Pili la Tathmini na Ufuatiliaji lililoandaliwa na Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo Kikuu cha Calfonia cha Marekani lililofanyika Jijini Dodoma.
2 (4)
Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Bw. Erick Kitali akisissitiza umuhimu wa Taasisi za Serikali kushirikiana na Ofisi hiyo katika kujenga  mifumo mbalimbali ili kuboresha huduma zinazotolewa kwa wananchi katika sekta ya afya  wakati wa hafla ya kufunga  Kongamano la Pili la Tathmini na Ufuatiliaji lililoandaliwa na Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo Kikuu cha Calfonia cha Marekani lililofanyika Jijini Dodoma.
4 (3)
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  ( TAMISEMI) Dkt. Zainab Chaula  akimkabidhi cheti cha ushiriki Afisa uhusiano wa Chuo  Kikuu Mzumbe Bi. Fatna Mfalingundi wakati wa hafla ya kufunga  Kongamano la Pili la Tathmini na Ufuatiliaji lililoandaliwa na Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo Kikuu cha Calfonia cha Marekani  lililofanyika Jijini Dodoma.
5 (2)
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  ( TAMISEMI) Dkt. Zainab Chaula   akimkabidhi cheti cha ushiriki mkuu wa Shule ya Menejimenti na Utawala Chuo Kikuu  Mzumbe Dkt. Eliza Mwakasangula wakati wa hafla ya kufunga  Kongamano la Pili la Tathmini na Ufuatiliaji lililoandaliwa na Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo Kikuu cha Calfonia cha Marekani  lililofanyika Jijini Dodoma.
6 (2)
Mmoja wa washiriki wa Kongamano la Pili la Tathmini na Ufuatiliaji lililoandaliwa na Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo Kikuu cha Calfonia cha Marekani akipokea cheti cha ushiriki kutoka  kwa  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya  ( TAMISEMI) Dkt. Zainab Chaula  kwa  lililofanyika Jijini Dodoma.
3 (3)
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  ( TAMISEMI) Dkt. Zainab Chaula  (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya washiriki wa   Kongamano la Pili la Tathmini na Ufuatiliaji  wakati wa hafla ya kufunga Kongamano hilo lililoandaliwa na Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo Kikuu cha Calfonia cha Marekani  na kufanyika  Jijini Dodoma .
Na; Mwandishi Wetu- Dodoma
Chuo Kikuu Mzumbe kimepongezwa kwa kuendesha kwa ufanisi  Kongamano la Pili la Tathmini na Ufuatiliaji linalowaleta pamoja wataalamu wa sekta ya afya, wahadhiri na
wanafunzi wa chuo hicho.
Akizungumza Jijini Dodoma wakati akifunga Kongamano hilo, Naibu Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia masuala ya Afya, Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa utaratibu wa kuwa na Kongamano hilo utasaidia kuunganisha Taasisi  za Serikali kwa kushirikiana na  Chuo Kikuu cha Mzumbe ili kutumia tafiti zinazofanywa katika kutatua changamoto zilizopo katika sekta ya afya.
“Tunatarajia washiriki wa kongamano hili kutumia taaluma zao kuleta matokeo makubwa katika maeneo wanayofanyia kazi” alisisitiza Dkt. Chaula
Akifafanua zaidi amesema kuwa, dhamira ya serikali ni kuona suala la tathmini na ufuatiliaji linapewa mkazo katika maeneo yote ya kazi ili kuleta matokeo chanya yatakayowanufaisha wananchi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bw. Erick Kitali amesema kuwa ni muhimu kwa taasisi za serikali kuja pamoja na kushirikiana katika kujenga mifumo mbalimbali itakayosaidia kuboresha maisha ya wananchi.
Aliongeza kuwa, kuna umuhimu mkubwa wa kushirikiana katika kutekeleza masuala mbalimbali ya sekta ya afya hasa katika suala la ujenzi wa mifumo kupitia katika mradi huo wa Tathmini na Ufuatiliaji unaotekelezwa na Chuo hicho.
Kongamano la pili la tathmini na ufuatiliaji limefanyika Jijini Dodoma na kuratibiwa na Chuo Kikuu Mzumbe kwa kushirikiana na Chuo Kikuu Calfonia cha Marekani ambapo Kongamano hilo limewaleta pamaoja Wataalamu wa tafiti, Wanafunzi na Wahadhiri wa Chuo hicho wakishirikiana na wataalamu kutoka chuo Kikuu cha Calfonia.

No comments :

Post a Comment