Thursday, September 27, 2018

RAIS MAGUFULI ATAJA SABABU ZA DARAJA LA TAZARA KUPEWA JINA LA MTENDAJI WA TANROADS, MHANDISI MFUGALE.


Tanzanian President John Pombe Magufuli speaks during a joint press conference with Kenyan President on October 31, 2016 at the State House in Nairobi. President Magufuli is in the country for a two-day state visit. / AFP / SIMON MAINA (Photo credit should read SIMON MAINA/AFP/Getty Images)
RAIS John Magufuli ametaja sababu ya daraja juu (Fly Over) ya Tazara kuitwa jina la Ofisa Mtendaji wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Mhandisi Patrick mfugale ‘Daraja la Mfugale’.
Wakati akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Daraja la Mfugale iliyofanyika leo tarehe 27 Septemba 2018  jijini Dar es Salaam, amesema uzalendo na uchapakazi wa Mhandisi Mfugale tangu alipoanza kuitumikia nchi katika masuala ya
ujenzi, ndiyo sababu ya daraja hilo kupewa jina lake.
 “Watalaamu wetu nchini waige mfano wa uchapakazi wa Mfugale, mfugale hakupendelewa ni haki yake, yako mengi aliyofanya kwa ajili ya nchi ametanguliza utanzania badala ya ubinafsi, wako wataalamu wetu wachache wamekuwa chanzo cha matatizo hapa nchini,” amesema Rais Magufuli
Rais Magufuli amesema imezoeleka kwa majina ya wanasiasa kutumika katika madaraja na barabara mbalimbali, lakini kwa sasa ameamua heshima hiyo kutoa kwa wataalamu wanaoshiriki ujenzi wa barabara na madaraja.
“Pamoja na sifa zote zilizotajwa hapa za kujenga daraja la Mkapa ambalo ni refu kuliko yaliyokuwepo katika Afrika Mashariki na kati, akajenga daraja la umoja na madaraja mengine,” amesema Rais Magufuli.

No comments :

Post a Comment