Saturday, August 18, 2018

SPIKA NDUGAI AONGOZA KIKAO CHA MAFUNZO YA KAMATI YA UONGOZI ZANZIBAR

  Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha mafunzo kwa Kamati ya Uongozi, Makamu Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge na Wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge. Kikao hicho kinaendelea kwa siku ya pili katika Ofisi ya Ndogo ya Bunge Zanzibar.anayefuata ni Spika Mstaafu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Pandu Kificho, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye ulemavu, Mhe. Jenister Mhagama, Katibu wa Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai, Naibu Spika, Mhe. Dkt. Tulia Ackson na Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Mhe. Hawa Ghasia


Wajumbe wa Kamati ya Uongozi, Makamu Wenyeviti na Wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge wakimsikiliza mtoa mada kutoka Idara ya Usalama, Ndugu Mluli Mahendeka katika semina ya kuwajengea uwezo inayofanyika katika Ofisi Ndogo ya Bunge, Zanzibar. Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha mafunzo cha mafunzo hayo.

No comments :

Post a Comment