Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia akinamama
waliojifungua katika wodi ya wazazi kwenye hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora
ya Kitete Agosti 18, 2018.
NA
TIGANYA VINCENT
WAZIRI
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ameahidi kuhakikisha
kuwa kiasi cha shilingi milioni 405.7 zilizobaki zinatolewa kwa ajili ya
ukamilishaji wa Chuo cha Afya cha Tabora ili kazi zilizobaki zimalizike na
kianze kutoa mafunzo.
Alisema lengo ni kuhakikisha
ikifika mwakani mwezi wa kwanza Chuo hicho kinaanza kutoa kozi ambazo
zitasaidia kuongeza wataalamu wa kada mbalimbali za afya.
Mhe. Majaliwa ametoa kauli
hiyo leo mjini Tabora baada ya kukagua majengo ya Chuo hicho ambayo yamekamika
asilimia 85 toka miaka mitatu iliyopita lakini bado hayajaanza kutumika katika
utoaji wa mafunzo.
Alisema atakutana na viongozi
wa Wizara ya Afya kwa ajili ya kuona jinsi ya kuleta fedha mapame za
kukamilisha maeneo yaliyobaki na kufanyia ukarabati sehemu zilizoanza
kuharibika kama vile vioo ambavyo vimeshaanza kupasuka.
Awali Mganga Mkuu wa Mkoa wa
Tabora Dkt. Gunini Kamba alisema mpaka sasa Mkandarasi ameshalipwa bilioni
3.295 na kiasi kilichobaki ni milioni 405.7.
Alisema mradi huo ulikuwa
unafadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 15 na
Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) asilimia 85.
Dkt. Kamba alisema kwa upande
wa ADB ilishakamilisha malipo yake yote katika mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na
kazi zilizokwisha fanyika zimefikia asilimia 85 bado upande wa Serikali.
Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa
Tabora Aggrey Mwanri alimwomba Waziri Mkuu kusaidia ili majengo ya Chuo hicho
yaanze kutumika kuliko kubaki bila wanachuo na kuwa katika hatari ya kuchakaa.
Alisema kuanza kazi kwa Chuo
hicho kutasaidia kupunguza tatizo la watumishi katika Hospitali ya Kitete kwa
kuwa wanachuo watakuwa wakiongeza nguvu wakati wa mafunzo kwa vitendo.
Mkuu
wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akitoa maelezo mafupi leo kabla ya
kumkaribisha Waziri Mkuu kwa ajili ya kuzungumza na watumishi na
viongozi mbalimbali wa Manispaa na Ofisi yake.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassimu Majaliwa akizungumza na
watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora na wa Manispaa ya Tabora
na viongozi mbalimbali leo ikiwa ni siku ya mwisho ya ziara yake Mkoani
humo.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa Chuo cha Afya katika hospitali
ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora ya Kitete Agosti 18, 2018. Wapili kulia ni
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri.(PICHA NA VINCENT TIGANYA OFISI
YA RAS TABORA)
No comments :
Post a Comment