Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhe. Kangi Lugola akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza,
Phaustine Kasike kabla ya kuingia kwenye Kikao cha Kamati ya Bunge Mambo
ya nje, Ulinzi na Usalama kinachofanyika leo Agosti 24, 2018, jijini
Dodoma. Kamati hiyo inakutana na watendaji wa Jeshi la Magereza na Idara
ya Wakimbizi.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Phaustine Kasike(kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu kabla ya kuanza kwa Kikao cha
Kamati ya Bunge Mambo ya nje, Ulinzi na Usalama leo Agosti 24, 2018,
jijini Dodoma.
Maafisa waandamizi wa Jeshi la
Magereza wakisalimiana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi
Lugola kama inavyoonekana katika picha kabla ya kushiriki kikao kazi cha
Kamati ya Bunge Mambo ya nje, Ulinzi na Usalama.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhe. Kangi Lugola(katikati) akijadiliana na Maafisa waandamizi wa Jeshi
la Magereza kabla ya kuanza kwa kikao kazi cha Kamati ya Bunge Mambo ya
nje, Ulinzi na Usalama, leo Agosti 24, 2018 katika Ukumbi wa Bunge
jijini Dododma
Picha zote na Jeshi la Magereza
No comments :
Post a Comment