NA ANDREW CHALE, MOI
RAIS Mstaafu wa awamu
ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
amemtembelea na kumjulia hali Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi
Kigwangalla aliyelazwa katika wodi maalum kitengo cha Taasisi ya mifupa MOI,
hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam kwa mara nyingine tena
leo Agosti 16, 2018.
Hii inakuwa ni mara ya
tatu kwa Dkt. Kikwete kumtembelea Dk Kigwangalla ambapo awali alimtembelea
Agosti 8,2018 alipokuwa amelazwa Wodi ya Mwaisela akipatiwa Matibabu ya awali
na juzi Agosti 15, 2018 katika wodi ya Taasisi Tiba ya Mifupa MOI.
Akiwa hospitaini hapo Dkt.
Kikwete ameweza kumjulia hali na kubadilishana nae mawazo mbalimbali huku
akimtakia nafuu ya haraka ili aendelee na majukumu yake ya kila siku na
akimpongeza kwa shughuli zake anazozifanya katika kuinua sekta ya Utalii pamoja
na kulinda rasilimali za Maliasili.
“Nikutakie kheri.
Nashukuru kwa kukuta unaendelea vizuri sasa na nilikuja ukiwa upo unaongea
ukiwa umelala kitandani na kwa sasa nimekuja tena umeweza kuimarika na hata
kutembea na kukaa kama hivi hongera sana” alieleza Kikwete wakati akimjulia
hali Waziri Kigwangalla wodini hapo.
Tayari jopo la
Madaktari bingwa wa MOI wamebainisha kuwa Dkt. Kigwangalla kwa sasa anaendelea
vizuri na muda wowote anaweza kuruhusiwa kurejea nyumbani ambapo kwa sasa
sehemu zilizobakia ni mkono wake wa kushoto ambao kila siku unaendelea
kuimarika.
Hata hivyo, Dkt.
Kigwangalla amemweleza Kikwete kuwa kwa sasa hali yake inaendelea kuwa vizuri
na muda wowote anaweza kuruhusiwa kurejea nyumbani huku akiendelea na
mazoezi kidogokidogo.
Aidha, jioni ya jana
Dkt. Kigwangalla ameweza kufanya mazoezi ya kutembea umbali wa zaidi ya
kilometa moja kuanzia kwenye viunga vya Hospitali hiyo na kuzunguka maeneo
yanayozunguka Muhimbili na baadae kupanda kwa kutumia ngazi katika jengo
anapopatiwa matibabu kwa miguu mpaka gorofa ya sita.
Waziri Dkt.
Kigwangalla alipata ajali ya gari mnamo Agosti 4, 2018 eneoa la Magugu Mkoani
Manyara akiwa katika ziara ya kikazi ambapo katika ajali hiyo iliyokuwa na watu
6, Afisa Habari wa Wizara hiyo Hamza Temba alifariki dunia huku watano
wakijeruhiwa akiwemo yeye.
Rais Mstaafu wa awamu
ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
akizungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamisi Kigwangalla kitengo cha
mifupa MOI anapopatiwa matibabu alipomtembelea kwa mara nyingine jana.
Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamisi Kigwangalla kitengo cha mifupa MOI anapopatiwa matibabu alipomtembelea kwa mara nyingine jana.(PICHA NA ANDREW CHALE)
No comments :
Post a Comment