Dkt. Kebwe anamsikiliza kwa
makini Mgeni wake baada ya kumkabidhi kitabu kinachoonesha maeneo ya
Uwekezaji Mkoani Morogoro (Morogoro Region Investment Guide).
Dkt. Kebwe akimkabidhi Sarah Cooke kitabu cha Uwekezaji.
Wakiwa Ofisini, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
Dkt. Kebwe anamsindikiza mgeni wake baada ya kukamilisha mazungumzo yao.
………………………
Na. Andrew Chimesela – Morogoro
Serikali ya Uingereza imeonesha
nia ya kushawishi wawekezaji nchini mwake kuja kuwekeza hapa nchini
hususan katika Mkoa wa Morogoro katika Sekta mbalimbali ikiwemo Sekta
ya
Kilimo, viwanda na Madini.
Hayo yamefahamika jana Julai 18
mwaka huu wakati wa mazungumzo yaliyofanyika Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa
Morogoro baina ya Balozi wa Uingereza hapa nchini Mhe. Bi. Sarah Cooke
na Dkt. Kebwe Stephen Kebwe Mkuu wa Mkoa huo.
Awali viongozi hao wawili walianza
mazungumzo yao kuhusu miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na Uingereza
hapa nchini hususan iliyopo Mkoani Morogoro ikiwemo miradi ya Elimu –
Educationa Programme for Results (EP forR), ambapo Mhe. Cooke
alisema nchi yake imeongeza ufadhili wake kutoka 34% mwaka 2012 hadi
70/% mwaka 2016.
Kwa upande wa Afya Balozi huyo
alisema katika Mkoa wa Morogoro, Uingereza imefadhili Vituo vya Afya
katika eneo linalolenga Mpango wa Uzazi kwa akina mama kupitia Mradi wa Population Service International (PSI) ambapo hadi sasa jummla ya akinamama 9,400 Mkoani humo wamefaidika na huduma hiyo.
Aidha, Viongozi hao wawili
walizungumzia ufadhili unaotolewa na Uingereza katika nyanja za Maji na
Usafi wa Mazingira ikiwemo Kampeni inayoendelea sasa Mkoani Morogoro ya usichukuliepoanyumbanichoo, Mkoa huo ukiwa ni Mkoa wa Majaribio katika Kampeni hiyo.
Pamoja na miradi mingine mingi
waliyoizungumzia , Viongozi hao pia waligusia miradi ya Sekta ya Kilimo
na Miundombinu. Kwa upande wa Sekta ya Miundombinu upo mradi wa IRAT
yaani Improving Rural Access in Tanzania ambapo Uingereza imefadhili matengenezo ya makaravati ya barabara ya Chagongwe – Kumbulu iliyopo Wialaya ya Gairo.
Baada ya kumaliza mazungumzo
kuhusu miradi inayofadhiliwa na nchi ya Uingereza, Mkuu wa Mkoa wa
Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe alimshukuru Balozi wa Uingereza kwa
Ufadhili wa miradi yote hiyo ukiwemo mradi mkubwa wa Upimaji na
umilikishaji wa Ardhi unaotekelezwa katika Wilaya za Kilombero, Ulanga
na Malinyi kupitia Land Tenure Support Programme.
Dkt. Kebwe ametumia fursa hiyo
kumweleza Balozi Sarah Cooke uwepo wa maeneo mazuri ya uwekezaji katika
Mkoa wa Morogoro na akawasilisha ombi kwa balozi huyo kushawishi
wawekezaji walioko nchini mwake kuja kuwekeza Mkoani Morogoro katika
sekta mbalimbali ikiwemo ya Kilimo, viwanda na uchimbaji wa madini ya
dhahabu na Graphite.
Balozi Sarah Cooke alionekana
kushawishika na ombi la mwenyeji wake na kuahidi kulifanyia kazi haraka
huku akiahidi kutafuta muda wa kufanya ziara katika Mkoa wa Morogoro kwa
lengo la kutembelea miradi wanayoifadhili lakini pia kutembelea maeneo
ya uwekezaji kama alivyokuwa ameombwa na mwenyeji wake.
No comments :
Post a Comment