Tuesday, July 17, 2018

TRA YAJA NA MKAKATI MAALUM KUONGEZA MAPATO KUPITIA SEKTA YA PICHA 1.

PICHA 1.

Kamishna wa Kodi za Ndani Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara ya Utalii (TATO), Bw. Wilberd Chambulo wakati wa ziara yake ya kikazi Jijini Arusha yenye lengo la kuongeza mapato ya Serikali kupitia sekta ya utalii nchini.

PICHA 2.

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Arusha, Bw. Faustine Mdesa (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara ya Utalii (TATO), Bw. Wilberd Chambulo wakati wa ziara ya kikazi ya Kamishna wa Kodi za Ndani Jijini Arusha yenye lengo la kuongeza mapato ya Serikali kupitia sekta ya utalii nchini.

PICHA 3.

Kamishna wa Kodi za Ndani Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya (kulia) akifanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara ya Utalii (TATO), Bw. Wilberd Chambulo wakati wa ziara yake ya kikazi Jijini Arusha yenye lengo la kuongeza mapato ya Serikali kupitia sekta ya utalii nchini.

PICHA 4.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara ya Utalii (TATO), Bw. Wilberd Chambulo (kushoto) akimwelezea jambo Kamishna wa Kodi za Ndani Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya pamoja na watendaji wengine wa TRA aliofuatana nao kuhusu namna sekta ya utalii nchini inavyochangia pato kubwa kwa Serikali wakati wa ziara ya kikazi ya Kamishna huyo Jijini Arusha yenye lengo la kuongeza mapato ya Serikali kupitia sekta ya utalii nchini.
(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-TRA)
 ………………………………..

Na Rachel Mkundai, Arusha
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imekuja na mkakati maalum wa kuhakikisha kwamba
pato la Serikali na kodi stahiki inapatikana kupitia sekta ya utalii nchini.
Akizungumza Jijini Arusha, Kamishna wa Kodi za Ndani, Bwana ELIJAH MWANDUMBYAamesema kwamba, sekta ya utalii ni moja ya sekta inayoiingizia Serikali fedha nyingi za kigeni na hivyo inahitaji mkakati madhubuti ili kuongeza pato kwa Serikali
“Sekta ya utalii inaingizia serikali fedha nyingi za kigeni, TRA tumekuja na mkakati maalum ili kuhakikisha kuwa sekta hii inachangia pato la taifa kupitia kodi stahiki kwa mujibu wa sheria za kodi”, amesema Kamishna wa kodi za ndani.
Mwandumbya ameongeza kuwa kwa muda mrefu sekta ya utalii imekuwa ikifanya vizuri lakini bado inahitaji mkakati wa kuhakikisha kwamba kila pato linaloingia kupitia sekta hii linaongeza tija kwenye mapato ya nchi kupitia kodi mbalimbali kama zilivyoainishwa na sheria za kodi.
Aidha, Kamishna Mwandumbya amefafanua kuwa moja ya mikakati hiyo ni kushirikiana na taasisi zingine za serikali zilizopo kwenye sekta ya utalii zikiwemo Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Chama cha wafanyabiashara wa Utalii  (TATO) pamoja na  Wizara ya Maliasili na Utalii na wadau wengine wanaojihusisha na utalii.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Bwana Allan  Kijazi amesema TANAPA ipo tayari kushirikiana na  TRA pamoja na taasisi zingine za serikali kwa kuwa lengo ni kukusanya mapato ya serikali na hivyo kuhakikisha kuwa mapato yanayopatikana kupitia utalii yatanufaisha nchi kwa kuleta  tija katika mapato.
“Sisi sote ni taasisi za serikali , tunajenga nyumba moja, tutashirikiana nanyi ili serikali yetu Isimame imara na kupata kodi stahiki”, amesema Bw Kijazi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara ya Utalii (TATO), Bwana Wilberd Chambulo amewataka Wafanyabiashara wanaojihusisha na masuala ya utalii kujenga utamaduni wa kulipa kodi kwa manufaa ya nchi ambapo pia ameunga mkono ujio wa mkakati huo maalum wa TRA wa kuongeza mapato kupitia sekta ya utalii.
Sekta ya utalii inatajwa kuwa moja ya sekta inayoiingizia Serikali fedha za kigeni hata hivyo takwimu zinaonesha kuwa kuna wafanyabiashara 2,200 wanaotambulika katika utalii nchini na kati ya hao 1,403 wanafanya shughuli zao katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga 
Hivyo, utekelezwaji wa mkakati huo utaipelekea Serikali kuongeza makusanyo ya mapato yake na kukuza maendeleo kwa wananchi katika kutoa huduma mbalimbali za kijamii.

No comments :

Post a Comment