Thursday, July 19, 2018

TBL FC KWENDA UINGEREZA KUTEMBELEA KLABU YA LIVERPOOL

????????????????????????????????????
Wachezaji wa timu ya TBL Group FC  ambao ni mabingwa wa  kombe la Standard Chartered 2018 wakiwasili makao makuu ya kampuni hiyo Ilala jijini Dar es Salaam  wakati wa hafla ya kupongezwa
????????????????????????????????????
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani (Kushoto) akiwa na maofisa wa benki hiyo pamoja na wafanyakazi wa TBL Group Ilala jijini Dar es Salaam wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa wa TBL Group na Rais wa kitengo cha ukuzaji wa Masoko wa ABinBev kanda ya Afrika Mashariki,Roberto Jarrin,wakati wa mkutano wa kupongeza wachezaji wa TBL FC
????????????????????????????????????
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani (Kushoto)   akifafanua jambo  katika mkutano huo
????????????????????????????????????
Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Masoko wa  benki ya Standard Chartered , Juanita Mramba,akitoa maelezo kuhusiana na ziara hiyo
????????????????????????????????????
Mkurugenzi Mkuu  wa TBL Group na Rais wa kitengo cha ukuzaji wa Masoko wa ABinBev kanda ya Afrika Mashariki, Roberto Jorrin ( kushoto) akiwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani (wa pili kulia ) pamoja na wachezaji wa timu ya TBL FC  wakishangilia kombe wakati wa hafla ya kuipongeza
TBL FC 14
Wafanyakazi wa TBL na Standard Chartered katika picha ya pamoja katika hafla ya kuipongeza TBL FC
………………….
TBL FC  Kwenda Uingereza  kutembelea klabu ya Liverpool
-Kushuhudia mechi ya ligi ya Uingereza Live
 

 
Bingwa wa mashindano ya soka ya makampuni yaliyoandaliwa na Benki ya Standard Chartered,
mapema mwezi uliopita,TBL FC, itaondoka nchini mwezi septemba 2018 kwenda nchini Uingereza,  kutembelea klabu maarufu ya Liverpool pamoja na  kukutana na wachezaji mashuhuri wanaochezea klabu hiyo.
 

 
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered, Sanjay Rughani,wakati alipofanya ziara makao makuu ya TBL Group Ilala jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuipongeza timu hiyo sambamba na kukutana na watendaji wakuu wa kampuni hiyo.Alibainisha kuwa watakuwa nchini Uingereza kati ya Novemba 8 na Novemba 10 ambapo pia watashuhudia mechi ya mchezo wa ligi kuu ya Uingereza , kati ya  timu ya Fullham na Liverpool utakaopigwa katika uwanja wa Anfield.
 

 
Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Group,Roberto Jarrin, aliipongeza benki ya Standard Chartered, nchini kwa ubunifu mkubwa  wa kuwaunganisha wateja wake kupitia Nyanja ya michezo sambamba na utoaji huduma bora kwa wateja wake.
 

 
Mashindano ya Standard Chartered 2018  yalifanyika mwezi uliopita na kushirikisha  timu za makampuni mbalimbali ambao ni wateja wa benki hiyo na kufanyika katika uwanja wa Gymkhana jijini Dar es Saalaam ambapo TBL FC, iliibuka na ushindi wa kuifunga timu ya kampuni ya Mwananchi Communication mabao 3-2 kwa njia ya penalti na kujihakikishia ubingwa wa michuano hiyo.
 

 

 
Nahodha wa timu hiyo,Lupa Mwanjopa,alitoa shukrani kwa mwandaaji wa mashindano hayo na kueleza kuwa wamefurahi kupata fursa hiyo ya kwenda nchini Uingereza sambamba na kutembelea klabu ya Liverpool na kukutana na wachezaji nguli wa timu hiyo “Michezo ni moja ya jukwaa la kuwaunganisha watu pamoja na kujenga afya,tunashukuru Benki ya Standard Chartered kwa kuipa umuhimu na kuwajali wateja wake”alisema.
 

 
Mkuu wa Uhusiano na Masoko wa Benki hiyo, Juanita Mramba, alisema kuwa mbali na kutembelea klabu hiyo pia watapata nafasi ya kufanya mazoezi katika akademi ya klabu hiyo katika uwanja wa Anfield pamoja na kutembelea maeneo mbalimbali ya uwanja huo  kabla ya kwenda kuangalia mchezo wa wapinzani wa Liverpool.

No comments :

Post a Comment