Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa
mwaka huu ,Charles Kabeho ,akitembelea na kujionea shughuli za
mapambano dhidi ya Ukimwi katika kituo cha afya Kerege ,Bagamoyo Mkoani
Pwani.
Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa ,Charles Kabeho akizindua kituo cha afya Kerege wilayani Bagamoyo.
Mkuu wa wilaya ya
Kibaha Assumpter Mshama (kulia) akimkabidhi mwenge wa uhuru mkuu wa
wilaya ya Bagamoyo alhaj Majid Mwanga (kushoto) wakati wa makabidhiano
hayo yaliyofanyika shule ya msingi Mapinga.
Picha na Mwamvua Mwinyi
……………….
NA MWAMVUA MWINYI,BAGAMOYO
BOHARI ya madawa (MSD), imeelekezwa kufanya
jitihada za kupeleka vifaa tiba vitakavyokidhi mahitaji ,katika kituo
cha afya Kerege kilichopo Bagamoyo, Mkoani Pwani ,ili kukabiliana na
tatizo la ukosefu wa vifaa tiba .
Kiongozi wa mbio za
mwenge kitaifa mwaka huu ,Charles Kabeho alitoa rai hiyo ,Kerege
wilayani Bagamoyo wakati alipokuwa akikagua na kujionea shughuli za
mapambano dhidi ya Ukimwi katika kituo hicho .
Alieleza ,,adhma ya
serikali ni kuona vituo vya afya vinaongezeka ,huduma za afya
zinaboreshwa hivyo MSD ihakikishe inasambaza vifaa hivyo na madawa ili
kuendana na malengo ya serikali .
Akizungumzia suala la
ugonjwa wa Ukimwi ,aliitaka jamii kujitambua kwa kupima afya zao na
ambao walishagundulika kuwa na VVU waendelee na dawa bila kupuuzia
masharti ya waatalamu wa afya.
Hata hivyo Kabeho alisisitiza ,ukimwi bado upo hivyo kila mmoja anawajibu wa kujali afya yake na kupambana na maambukizi mapya.
Akitoa taarifa ya
mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Kerege ,mganga mkuu wa wilaya hiyo,
Silivia Mamkwe alisema hadi sasa mradi huo umegharimu kiasi cha
sh.milioni 561 ambapo mil.500 ni fedha kutoka OR-TAMISEMI .
“Kiasi cha sh.mil.44
ni mchango wa halmashauri ,mil.11.353 ni mchango wa wadau ,mil.4.147
wananchi na mil .1.5 kupitia nguvu kazi “.
Silivia alisema,
lengo la mradi ni kuboresha huduma za afya ,dharura na upasuaji wa
wajawazito ambapo huduma za upasuaji wa dharura zimesogezwa karibu na
wananchi kupunguza vifo vya mama na watoto .
Alisema ,mradi
ulianza kutekelezwa oktoba mwaka jana na kwasasa majengo matano
,miundombinu mitano vimekamilika kwa asilimia 100,huku wakitarajia
kufikia wananchi 8,921#.
“Majengo mawili la kuhifadhi maiti na jengo la kufulia yamekamilika kwa asilimia 80” alifafanua.
Awali akipokea mwenge
wa uhuru kutoka Kibaha Vijiji ,Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo alhaj Majid
Mwanga alisema ,mwenge huo utapitia miradi 12 iliyogharimu sh.bilioni
10.8.
Alhaj Mwanga alielezea, miradi miwili itakaguliwa na miradi kumi itawekewa mawe ya msingi.
Mwenge wa uhuru
unaendelea na shughuli zake Mkoani Pwani ,ikiwa umefikia halmashauri ya
saba kati ya tisa na wilaya ya tano kati ya saba za mkoani hapo.
No comments :
Post a Comment