Thursday, July 19, 2018

KONGAMANO LA SIKU MBILI SEKTA YA MAJI


Pix 00
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo kwa wadau wa sekta ya maji (hawapo pichani) wakati wa kongamano la kujadili fursa zilizopo na changamoto zinazoikabili sekta binafsi nchini katika kuchangia maendeleo ya sekta ya maji nchini.
Pix 01 b Pix 01
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo kwa wadau wa sekta ya maji wakati wa kongamano la kujadili fursa zilizopo na changamoto zinazoikabili sekta binafsi nchini katika kuchangia maendeleo ya sekta ya maji nchini.
Pix 02
Naibu Waziri wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya akizungumza na wadau wa sekta ya maji wakati wa kongamano la kujadili fursa zilizopo na changamoto zinazoikabili sekta binafsi nchini katika kuchangia maendeleo ya sekta ya maji nchini.
Pix 03
Baadhi ya wadau wa sekta ya maji wakiwa katika kongamano la kujadili fursa zilizopo na changamoto zinazoikabili sekta binafsi nchini katika kuchangia maendeleo ya sekta ya maji nchini.
Pix 04
Mwakilishi toka sekta binafsi nchini (TPSF) Louis Akaro akizungumza na wadau wa sekta ya maji wakati wa kongamano la kujadili fursa zilizopo na changamoto zinazoikabili sekta binafsi nchini katika kuchangia maendeleo ya sekta ya maji nchini.
Pix 05
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Viwanda toka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Aristide Mbwasi akizungumza na wadau wa sekta ya maji wakati wa kongamano la kujadili fursa zilizopo na changamoto zinazoikabili sekta binafsi nchini katika kuchangia maendeleo ya sekta ya maji nchini.
Pix 06
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa sekretarieti ya maandalizi ya kongamano la kujadili fursa zilizopo na changamoto zinazoikabili sekta binafsi nchini katika kuchangia maendeleo ya sekta ya maji nchini.
Pix 07
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa (wa pili toka kulia) akipata maelekezo toka kwa Afisa Mauzo wa kampuni ya Pipe Industries Ltd. Ezra Chiwelesa wakati wa kongamano la kujadili fursa zilizopo na changamoto zinazoikabili sekta binafsi nchini katika kuchangia maendeleo ya sekta ya maji nchini, Kushoto ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo Piyush Nath na wapili toka kushoyo ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso.
Pix 08
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa akipata maelekezo ya vifaa vya maji  toka kwa Afisa Mauzo wa kampuni ya Plasco Ltd. Mhandisi Elisaria Aminiel wakati wa
kongamano la kujadili fursa zilizopo na changamoto zinazoikabili sekta binafsi nchini katika kuchangia maendeleo ya sekta ya maji nchini.
Picha na MAELEZO
…………..

Kaulimbiu- “Kuimarisha Ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi katika Kuendeleza Sekta ya Maji Nchini.” (19 – 20/07/2018)
Moto – Maji ni Uchumi
Wizara ya Maji na Umwagiliaji katika kutekeleza Program yake ya Pili (Water sector Development Program II) – WSDP II) imeandaa Kongamano la siku mbili katika Ukumbi wa JNICC, Dar es Salaam ambapo imewakutanisha wadau wa sekta ya Maji.
Walioshirikishwa ni watendaji wakuu wa Idara za serikali sekta ya maji na Viwanda, Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma (MDAs; Washiriki wa Maendeleo (Development Partners) , Wakandarasi, Wawekezaji katika sekta ya Maji, mfano Water Aid, PIPE, Kiboko Plastics, Kamal Steels; Wakandarasi; Washauri ; Sekta Binafsi (TPSF).
Meza Kuu Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa, alifuatana na Naibu Waziri wake na Katibu Mkuu na Naibu katibu Mkuu wake; Naibu W#aziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Stela Manyaya (MB),ambaye naye pia alifuatana Katibu Mkuu na naibu wake kutoka Wizara yake ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.
Pia meza kuu ilikuwa na Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Miradi la Uingereza (DFDI) wakati chombo cha wawakilishi wa sekta binafsi (TPSF) kiliwakilishwa.
Mh. Profesa Mbalawa amefungua Kongamano kwa kutoa onyo kwa watendaji wa sekta ya Maji kwa kuwataka watende kazi kwa akilini na uweledi na waache vitendo vya ubabaishaji. Ametoa mfano kuwa kwa muda mfupi aliokaa Wizara hiyo ya Maji na Uwekezaji amegundua miradi mingi kutekelezwa kwa uzembe, kutoa tenda kwa makandarasi wasiokuwa na uwezo, wasimamizi kutosimamia vizuri miradi na waandalizi wa miradi kuandaa ovyo miradi kutokana labda kuwa na uwezo mdogo ama kulipua kazi.
amesema  serikali inaamini itakamilisha lengo lake la kufikia malengo ya melinia (2015 – 2020) kama ilivyojizatiti na hivyo ni wajibu wa kila mtendaji wa sekta ya maji kujipanga kwa nafasi yake kwa kuhakikisha anatimiza wajibu wake na kuonya kuwa yule asiyeweza ni bora awapishwe wanaoweza ili pasiwepo na kukwama kwa yale yaliyokusudiwa kutekelezwa.
Waziri Prof Mbawara amesema katika Programu ya Kwanza (WSDP I) serikali ililenga kuacha mwelekeo wake wa kuendesha miradi ya maji yenyewe na kushirikisha sekta binafsi. Programi hiyo iliyoanza Julai 2007 – 2016) ilishirikisha sekta binafsi katika kubuni kupanga na kujenga miundombinu ya maji lakini tadhmini yake emona mafanikia madogo.
Programu ya kwanza iliyotumia trilioni 3.076 iligundua mapungufu ya baadhi ya miradi kutokamilishwa; kujengwa lakini kutokuwa katika viwango vya ufanisi; ama kuchukua muda mrefu mno kukamilika.
Lengo kuu sasa katika Programu hii ya pili ni kuona kuwa kuna kasi ya utekelezaji wa miradi na kuona kuwa inatekelezeka kwa ufanisi unaokusudiwa, kadhalika kushirikisha sekta binafsi katika kubuni, kupanga kujenga (miundombinu) na kutoa huduma ya maji.
Matarajio yake ni kuwa Kongamano hili la siku mbili ni kuja na mapendekezo ya kuleta nguvu moja baina ya serikali na sekta binafsi katika kufanikisha malengo ya serikali katika sekta ya maji.
Kwa upande wake Naibu waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Stella Manyanya, amehimiza wawekezaji, wafanyabiashar na wananchi kwa jumla kusoma andiko la serikali linalolenga kuleta mageuzi makuwa katika sekta ya biashara na uwekezaji, ambapo serikali kwa kushirikisha sekta binafsi imepitia sera, sheria, mifumo na miongozo  inayosimamia sekta ya biashara, viwanda na uwekezaji na kubainaisha kero na changamoto ambazo zinakusudiwa kuondolewa.
Majadiliano yameendelea mchana wa leo na washiriki wataendelea na kesho kujadili jinsi ya sekta binafsi kuboresha mahusiano na kubuni mawazo mapya katika kufanikisha sekta binafsi kutoa huduma ya maji ambapo kwa sasa huduma hizo zinatolewa na serikali kupitia chombo chake cha mamlaka za huduma za maji mijini.

No comments :

Post a Comment