Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi
Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro Mhe. Elizabeth Nyembele akizungumza na
waandishi wa habari leo wakati walipotembelea katika Mahakama ya Hakimu
Mkazi Morogoro kwenye moja ya ziara za kimafunzo wakiwa katika semina
ya Waandishi wa habari za mahakama mkoani Morogoro
Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi
Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro Mhe. Elizabeth Nyembele akizungumza na
wananchi waliokuwa wakisubiri kuanza kwa mashauri yao kwenye Mahakama
ya Hakimu Mkazi Morogoro katika ziara ya kimafunzo kwa waandishi wa
habari wakiwa kwenye semina ya uandishi wa habari za mahakama mkoani
Morogoro
(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-MOROGORO)
Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi
Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro Mhe. Elizabeth Nyembele akizungumza na
waandishi wa habari katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro kwenye
ziara ya kimafunzo kwa waandishi wa habari wakiwa kwenye semina ya
uandishi wa habari za mahakama mkoani Morogoro
Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi
Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro Mhe. Elizabeth Nyembele akionyesha
waandishi wa habari nembo ya iliyopo kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi
Morogoro kwenye ziara ya kimafunzo kwa waandishi wa habari wakiwa
katika semina ya uandishi wa habari za mahakama mkoani Morogoro
Baadhi ya waandishi wa habari
wakisikiliza maelezo ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi Mahakama ya
Hakimu Mkazi Morogoro Mhe. Elizabeth Nyembele hayupo kwenye picha.
Mtendaji Mkoa wa Mahakama
Nestory Mjunangoma amesema akitoa maelezo kwa waandishi wa habari wakati
alipokuwa akitoa ufafanuzi wa mambo kadhaa kwa wanahabari.
Baadhi ya wanahabari wakiendelea na ziara yao.
Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi
Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro Mhe. Elizabeth Nyembele akimsikiliza
mmoja wa waandishiwa habari wakati wa ziara hiyo ya kimafunzo.
……………………………………………………………………………………….
Na Lilian Lundo na Beatrice Lyimo-MAELEZO, Morogoro
Waandishi wa habari za Mahakama
wamefanya mafunzo kwa vitendo katika Mahakama za Mkoa wa Morogoro ili
kuona namna Mahakama hizo zinavyotekeleza majukumu yake ya kila
siku.
Lengo la mafunzo hayo ni
kuhakikisha wadau wa mahakama wakiwemo waandishi wa habari wanakuwa na
uwezo wa kuwahudumia wananchi kwa weledi.
Akitoa maelekezo namna mahakama
zinavyofanya kazi, Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu
Mkazi Morogoro Mhe. Elizabeth Nyembele amesema kuwa , katika mahakama
zipo kesi zinazosikilizwa katika Mahakama za wazi na nyingine
husikilizwa Mahakama za ndani( Chamber).
” Kesi zote zinazohusu
unyanyasaji wa kijinsia mfano ubakaji, kesi za mambo ya ndoa au kesi
yoyote ambayo itamhusisha mtoto kesi zao husikilizwa katika mahakama za
ndani ( Chamber)” ameongeza Mhe. Hakimu Nyembele.
Aidha, Mhe. Hakimu Nyembele
amesema kuwa kwa mkoa wa Morogoro wamekuwa wakipokea kesi nyingi
zinazohusiana na masuala ya unyang’anyi, madawa ya kulevya na ujangili
unaosababishwa na mkoa huo kuzungukwa na mapori.
Akizungumza kuhusu suala la
rushwa kwa makarani wa mahakama, Mhe. Nyembele ametoa rai kwa watumishi
wote wa mahakama kuepuka kupokea rushwa na kuwa waaminifu katika
utendaji wao.
Vilevile amesema kuwa katika
kudhibiti suala la rushwa katika mahakama nchini, mahakama imetoa elimu
kwa umma pamoja na matangazo ya huduma mbalimbali za kimahakama
zinazotolewa bure mfano nakala za hukumu.
Kwa upande wake, Hakimu Mkazi
Mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Morogoro Mjini Mhe. Agnes Ringo amesema
kuwa kwa sasa kuna utaratibu mpya wa namna kesi za watoto
zinavyoendeshwa bila kutoa utambulisho rasmi wa mtoto husika.
Nae Mtendaji Mkoa wa Mahakama
Nestory Mjunangoma amesema kuwa katika mkakati wa kuboresha huduma za
mahakama, Mahakama mkoa wa Morogoro inatarajia kuanza ujenzi wa ghorofa
nne katika mwaka huu wa fedha zitakazokuwa na huduma zote za kimahakama
kuanzia Mahakama ya Mwazo hadi Mahakama Kuu.
Aidha, Mjunangoma ameongeza kuwa ujenzi huo unatarajiwa kukamilika mwaka 2020.
Mafunzo hayo ni moja ya mradi wa
maboresho ya huduma za mahakama inayotekeleza programu mbalimbali chini
ya mpango mkakati wa mahakama wa miaka mitano 2015/2016-2019/202
iliyoandaliwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama chini ya ufadhili wa Benki
ya Dunia.
No comments :
Post a Comment