Kamishna Jenerali wa Magereza,
Phaustine Kasike akizungumza na Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim
Juma alipomtembelea Ofisini kwake leo Julai 19, 2018 jijini Dar es
Salaam kwa lengo la kujitambulisha rasmi tangu aapishwe kuwa Mkuu wa
Jeshi la Magereza Tanzania Bara, Julai 14, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Phaustine Kasike (kulia) akisalimiana na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya
Tanzania, Bw. Hussein Kattanga alipotembelea Ofisi ya Jaji Mkuu wa
Tanzania jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Phaustine Kasike wakiteta mambo mbalimbali juu ya ushirikiano wa vyombo
hivyo muhimu katika kusimamia sheria na haki. Kulia ni Jaji Mkuu wa
Tanzania, Prof. Ibrahim Juma(kushoto) ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya
Tanzania, Bw. Hussein Kattanga.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Phaustine Kasike akiagana na Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma
baada ya mazungumzo ambapo Kamishna Jenerali wa Magereza ameahidi kutoa
ushirikiano kwa Vyombo vyote vya Haki jinai ili kutimiza majukumu yake
ipasvyo
Picha zote na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Makao Makuu ya Jeshi la Magereza).
No comments :
Post a Comment