Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP
Simon Sirro akiwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza kwa ajili ya
ziara ya kikazi kwenye baadhi ya mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP
Simon Sirro akiwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna
wa Polisi (DCP) Ahmed Msangi (Kulia) na Afisa Mnadhimu wa Mkoa huo
Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Advera Bulimba (Kulia) baada ya
kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza kwa ajili ya ziara ya kikazi
kwenye baadhi ya mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP
Simon Sirro akipokea Salam ya heshima baada ya kuwasili Makao Makuu ya
Polisi Mkoa wa Mwanza kwa ziara ya kikazi katika baadhi ya mikao ya
Kanda ya Ziwa.Kushoto ni Kamanda wa mkoa huo, Naibu Kamishna wa Polisi
DCP Ahmed Msangi
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP
Simon Sirro akimfariji Bi Lily Matola ambaye ni Afisa Mnadhimu Mstaafu
wa Polisi mkoani Mwanza baada ya kufiwa na Mume wake Marehemu Edmund
Matola. IGP Sirro yupo ziara ya kikazi katika mikoa ya Kanda ya Ziwa
kuangalia
utendaji wa Polisi hususani katika kupunguza ajali za
barabarani nchini
Picha na Jeshi la Polisi
……………….
Na. Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP
Simon Sirro amewasili mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi na Julai 5
mwaka huu anatarajiwa kufunga mafunzo katika Chuo cha Polisi Wanamaji
Mwanza ambayo yana lengo la kukabiliana na uhalifu unaotokea katika
Bahari, Maziwa na Mito hapa nchini.
Pamoja na ufungaji wa mafunzo hayo
pia ataendelea na ziara ya kukagua utendaji wa Polisi katika baadhi ya
mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa lengo la kuhakikisha uhalifu unapungua hapa
nchini ikiwemo ajali za barabarani, Maujai ya kishirikina na uhalifu
katika Visiwa vilivyopo Ziwa Viktoria.
Mapema baada ya kuwasili
amezungumza na Maofisa wa Polisi waliopo Mkoani Mwanza na kusisitiza
kufanya kazi kwa weledi pamoja na kuhakikisha kuwa ajali zinapungua
katika maeneo yao.
“Nimekuja kukagua utendaji wenu
ili kutatua baadhi ya changamoto zinazowakabili ili kufikia malengo
tuliyojiwekea ya kuhakikisha uhalifu unapungua hapa nchini, hivyo ni
imani yangu kila mmoja atawajibika kwa nafasi yake na kuwasimamia
waliopo chini yake ipasavyo” Alisema IGP Sirro
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi DCP Ahmed Msangi amesema hali ya
usalama katika mkoa huo ni shwari na suala la usalama barabarani
linaendelea kusimamiwa kikamilifu kwa kushirikiana Mamlaka nyingine
zinazohusika.
No comments :
Post a Comment