Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohamed Khamis
Baucha (kushoto) akiongea wakati wa kukabidhi zawadi kwa washindi wa
Promosheni ya Ni Jero Yako Tu jana. Kulia ni Rukia Mtingwa, Meneja
Mawasiliano wa Zantel Tanzania.
Washindi wa gari, pikipiki na baiskeli kwenye picha ya pamoja.
Washindi wa gari, pikipiki na baiskeli kwenye picha ya pamoja.
Na Mwandishi Wetu.
Kampuni ya mawasiliano ya Zantel
imekabidhi zawadi ya magari 2, pikipiki 5, baiskeli 8 na simu 2 kwa
washindi wa promosheni iliyomalizika karibuni iitwayo ‘Ni Jero Yako tu’
ambayo
iliwapa nafasi wateja wake wa Zanzibar nafasi ya kujishindia
magari, pikipiki, baiskeli,fedha taslimu na simu za kisasa za interneti
ya 4G.
Promosheni ya ‘Ni Jero Yako tu’ ya
kampuni ya Zantel ,imefanyika kwa kipindi cha miezi mitatu kwa lengo la
kuwashukuru wateja wake kwa kuendelea kuiunga mkono hususani katika
kipindi ambacho ilikuwa katika mchakato wa kuimarisha miundombinu yake
ya mawasiliano na wateja walishiriki promosheni hii kwa kununua vocha ya
muda wa maongezi ya shilingi 500/-.
Hadi kufikia mwisho wa promosheni
hii ambayo ilianza mapema mwaka huu, ikiwa imewalenga wateja wa
Zanzibar, wateja 3 wameweza kushinda magari kwa kila mmoja aina ya
Suzuki Carry, maarufu kama KIRIKUU, wateja 5 wamejishindia pikipiki kila
mmoja, wateja 40 walijishindia baiskeli, wateja 90 kila mmoja
alijishindia fedha taslimu shilingi 50,000/-na wateja 90 walijishindia
simu za mkononi za kisasa.
Akiongea wakati wa hafla ya
kukabidhi zawadi kwa washindi iliyofanyika katika ofisi za Zantel za
Zanzibar, Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohammed Khamis Mussa (Baucha)
alisema,”Tunawashukuru wateja wetu kwa kuendelea kutuamini na kutuunga
mkono, ndio sababu mwaka huu tuliwaletea promosheni ya kuwawezesha
kujishindia zawadi zinazoweza kubadilisha Maisha yao kwa namna moja ama
nyingine.”
“Zawadi tulizowapatia washindi
wetu wa leo zinaweza kuwasaidia kujiongezea pato la familia, hizi
Kirikuu pamoja na pikipiki wanaweza kuzitumia kufanya biashara ya
usafiri na kujiongezea kipato na ndio maana tumekuja na promosheni zenye
kutoa zawadi zinazolenga kuwanufaisha wateja wetu kiuchumi.”
Akizungumza baada ya kukabidhiwa
zawadi ya gari Bi Fatma Mohammed Haji mkazi wa Magomeni Unguja
alishukuru kampuni ya Zantel kwa kubuni promosheni zinazolenga
kuwasaidia wateja wake hasa Zanzibar kumzawadia gari baada ya kushiriki
kwenye promosheni ya Ni Jero Yako, aliongeza kuwa anatarajia kutumia
gari hiyo kufanyia biashara ya kusafirisha mizigo.
“Nawasihi wateja wengine wa Zantel
waendelee kushiriki kwenye promosheni mbali mbali za Zantel sababu
promosheni hizi ni za kweli na wao wanaweza kuibuka washindi kama mimi,”
alisema.
Hadi kufikia mwisho wa promosheni
hii, wateja 235 wa Zantel walifanikiwa kujishindia zawadi mbalimbali na
waliokabidhiwa zawadi jana ndio walikuwa wanahitimisha promosheni ya ‘Ni
Jero Yako Tu’.
Wakati huohuo, kampuni ya Zantel
inaendelea na promosheni inayojulikana kama “Tunaliamsha Kivingine”
ambayo imezinduliwa hivi karibumi baada ya kampuni kuboresha miundombinu
yake ya mawasiliano. Kupitia promosheni hii, wateja wa Zantel
wamewezeshwa kufurahia huduma za internet yenye kasi kubwa kwa gharama
nafuu kabisa.
No comments :
Post a Comment