Wednesday, July 18, 2018

HOSPITALI YA KITETE KUPATA MILIONI 300 KUKAMLISHA JENGO YA UPASUAJI


PIX 1
NA RS -TABORA
18 JULAI 2018
SERIKALI inatarajia kutatoa shilingi milioni 300 kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora (Kitete) kwa ajili kukamilisha chumba cha upasuaji na uboreshaji wa maeneo mengine.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu alipotembelea Hospitali hiyo kwa ajili ya kujionea hali ya utoaji wa
huduma za afya mkoani humo.
Alisema sehemu ya fedha itasaidia kuhakikisha inapanua chumba cha wazazi na wodi ya upasuaji kwa ajili ya kuboresha zaidi hizo hizo Hospitalini hapo.

Waziri huyo alisema watahakikisha wanapeleka fedha hizo kabla ya Mwezi Desemba mwaka huu ili kuhakikisha mwanamke anapojifungua anakuwa salama yeye na mtoto wake.

Aidha,aliwaagiza viongozi wa hospitali hiyo kuwa wabunifu kwa kununua vifaa vyote muhimu vinavyowezekana kuliko kusubiri Wizara kuwaletea kwa ajili ya kuhakikisha huduma muhimu zinakuwepo na wananchi wanapata matibabu kwa gharama nafuu.


Hata hivyo aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na miiko ya utumishi wa umma ili kuondoka malalamiko kwa wananchi wanaofika kupata huduma katika hospitali hiy.

Alisema uongozi wa Hospitali hiyo usimuone haya mtumishi ambaye ataonyesha vitendo vya ubaguzi na utoaji wa lugha chafu kwa wagonjwa wakati wa kutoa huduma.

Naye Mbunge wa Viti Maalumu CCM Mkoa wa Munde Tambwe aliupongeza Uongozi wa Hospitali ya Kitete kwa kuboresha hali ya usafi katika wodi mbalimbali na kusema hivyo mazingira ya wodini ni mazuri hakuna harufu kama siku za nyumba.

Alimuomba Waziri huyo mwenye dhamana na masuala ya afya kuwaongezea watumishi kutokana na kuzidiwa na wagonjwa , hali inayowafanya wananchi kuchelewa kupata huduma ya matatibabu.

Munde alisema hali hiyo ndio imepelekea baadhi ya wagonjwa kulalamikia kuwa kuna huduma mbaya kumbe watumishi wamezidiwa.

No comments :

Post a Comment