Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA
kutoka Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw.
Erick Kitali akisisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili kwa waweka
hazina na wahasibu wa mikoa ya Njombe, Songwe, Katavi na Mbeya wakati
akifungua awamu ya pili ya mafunzo ya matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2
yanafanyika jijini Mbeya.
Mkuu wa Timu ya Mifumo kutoka
mradi wa uimarishaji mifumo katika sekta za umma (PS3) Bw. Desderi
Wengaa akitoa maelezo ya awali kuhusu faida za mifumo mbalimbali
iliyojengwa na Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) na PS3 ili kuongeza tija katika kuwahudumia wananchi katika
mamlaka za Serikali za Mitaa, mafunzo hayo waweka hazina na wahasibu wa
mikoa ya Njombe, Songwe , Katavi na Mbeya wakati wa hafla ya kufungua
awamu ya pili ya mafunzo ya matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2 yanafanyika
jijini Mbeya.
Sehemu ya waweka hazina na
wahasibu wa mikoa ya Njombe, Songwe , Katavi na Mbeya wakifuatilia
hotuba ya mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA kutoka
Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Erick
Kitali wakati wa hafla ya kufungua awamu ya pili ya mafunzo ya matumizi
ya mfumo wa Epicor 10.2 yanafanyika jijini Mbeya.
Mweka hazina wa Halmashauri ya
Wilaya ya Tunduma Bw. Onesmo Raphael ambaye alikuwa Mwenyekiti wa
mafunzo ya siku nne kuhusu matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2 kwa waweka
hazina na wahasibu wa mikoa ya Njombe, Songwe , Katavi na Mbeya
akimkaribisha mgeni rasmi ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA
kutoka Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Bw. Erick Kitali wakati wa hafla ya kufungua mafunzo hayo yanafanyika
jijini Mbeya.
Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA
kutoka Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Bw. Erick Kitali (kulia) akifurahia jambo na Mkuu wa Timu ya Mifumo
kutoka mradi wa uimarishaji mifumo katika sekta za umma (PS3) Bw.
Desderi Wengaa mara baada ya hafla ya ufunguzi wa mafunzo kwa waweka
hazina na wahasibu wa mikoa ya Njombe, Songwe , Katavi , awamu ya pili
ya mafunzo ya matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2 yanafanyika jijini Mbeya.
Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA
kutoka Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Bw. Erick Kitali akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya washiriki wa
mafunzo ya wahasibu na waweka hazina wa mikoa ya Njombe, Songwe, Katavi,
awamu ya pili ya mafunzo ya matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2
yanafanyika jijini Mbeya.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo kama wanavyoonekana katika picha.
Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA
kutoka Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Bw. Erick Kitali akisisitiza jambo kwa wahasibu na waweka hazina wa
mikoa ya Njombe, Songwe, Katavi, awamu ya pili ya mafunzo ya matumizi ya
mfumo wa Epicor 10.2 yanafanyika jijini Mbeya.
Mweka hazina wa halmashauri ya
Wilaya ya Mpanda Bw. Mabula Mponeja akisisitiza jambo wakati wa mafunzo
kwa wahasibu na waweka hazina wa mikoa ya Njombe, Songwe, Katavi, awamu
ya pili ya mafunzo ya matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2 yanafanyika
jijini Mbeya.
(Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO, Mbeya
……………..
Na: Frank Mvungi- MAELEZO, Mbeya
Serikali imewaagiza Wahasibu na
Waweka Hazina kusimamia kikamilifu fedha zinazotolewa kwa ajili ya
miradi ya maendeleo katika Halmashauri zao kote nchini kwa kutumia
mifumo ya
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) iliyopo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa
TEHEMA kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(OR-TAMISEMI), Bw. Erick Kitali, wakati akifungua awamu ya pili ya
mafunzo ya siku nne kuhusu matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2 kwa wahasibu
na waweka hazina wa mikoa ya Njombe, Songwe, Katavi na Mbeya. Mafunzo
hayo yanafanyika jijini Mbeya ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kwa
kushirikiana na wadau wa maendeleo kuimarisha mifumo ili kuongeza tija
katika huduma zinazotolewa kwa wananchi.
“Kama mweka hazina au mhasibu
lazima uwe mstari wa mbele kuhakikisha kuwa kila eneo ambalo kuna fedha
za Serikali mnazisimamia kikamilifu kwakuwa hakuna atakayevumiliwa kwa
kushindwa kutekeleza majukumu yake vyema kwa kutumia mifumo hii ambayo
imeimarishwa kwa maslahi ya Taifa,” alisisitiza Kitali.
Mfumo wa Epicor 10.2 uko chini ya
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), na
umejengwa kwa kushirikiana na Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za
Umma (PS3) unaofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika la
Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID). Mradi huu wa miaka mitano
unatekelezwa katika mikoa 13 ya Tanzania bara.
Akifafanua, Bw. Kitali amesema
kuwa washiriki wa mafunzo hayo wana jukumu kubwa la kuelewa matumizi ya
mfumo wa Epicor 10.2 kwa ufasaha katika kipindi chote cha mafunzo, ili
kuepuka kutekeleza majukumu yao kinyume na taratibu za mifumo hii ambayo
kwa sasa imeunganishwa na kuweza kuongea ili kurahisisha utendaji na
kuchochea maendeleo endelevu.
Kwa upande wake, Mkuu wa Timu ya
Mifumo kutoka Mradi wa PS3, Bw. Desderi Wengaa, amesema kuwa OR-TAMISEMI
imekuwa ikifanya kazi kubwa kwa kushirikiana na mradi huo katika
kuimarisha mifumo ikiwemo wa Epicor 10.2.
Aliongeza kuwa mifumo yote sasa
imeunganishwa hadi ngazi ya watoa huduma, hali inayosaidia kuimarisha
utoaji wa huduma kwa wananchi na hivyo kusaidia kuongeza uwazi na
uwajibikaji katika ngazi za vituo vya kutolea huduma.
Kutokana na kuimarishwa kwa mifumo
hiyo, Serikali imeweza kuongeza ukusanyaji wa mapato na huduma
zinazotolewa kwa wananchi katika vituo vya kutolea huduma zikiwemo za
afya na elimu.
Akizungumzia lengo la mafunzo ya
matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2, Bw. Wengaa alieleza kwamba ni
kuwajengea uwezo wahasibu na waweka hazina kusimamia rasilimali fedha
kikamilifu katika maeneo yao ili dhamira ya Serikali kuwahudumia
wananchi kwa kutoa huduma bora itimie.
Mafunzo hayo yanayoendeshwa na
OR-TAMISEMI kwa kushirikiana na Mradi wa PS3, yameingia katika awamu ya
tatu wiki hii, baada ya awamu ya kwanza nay a pili kufanyika wiki
iliyopita. Licha ya Mbeya, mfunzo kama haya yanayohusisha washiriki
kutoka nchi nzima yanaendelea pia katika vituo vingine, ambavyo ni mikoa
ya Iringa, Dodoma, Mwanza, Mtwara na Kagera.
No comments :
Post a Comment