Mshauri wa Masoko wa Kampuni ya
nishati ya nguvu ya jua Mobisol,Livinus Manyanga, akikata utepe kuzindua
luninga kubwa inayotumia umeme wa juakwenye moja ya maduka yao jijini
Arusha,wengine pichani ni Maofisa waandamizi wa kampuni hiyo.
Meneja Masoko wa Mobisol,Seth Matemu akionyesha bidhaa bora za kampuni hiyo
Mshauri wa Masoko wa Kampuni ya nishati ya nguvu ya jua Mobisol,Livinus Manyanga,akiongea na waandishi wa habari
…………………………………………………………………..
Katika kukidhi mahitaji ya wateja wake wanaoishi maeneo yasio na umeme
wanaohitaji televisheni kubwa,kampuni inayoongoza kwa kutoa huduma za
umeme wa jua na kuuza bidhaa bora zinazotumia nishati hiyo, Kampuni ya
Mobisol imezindua televisheni bapa kubwa yenye kioo
cha kisasa ya Inchi
43 katika soko la Tanzania.
Televisheni
yenye ukubwa huu na inayotumia umeme unaotokana na nishati ya jua ni
kwa mara ya kwanza, imezinduliwa katika soko la Tanzania, kwa ajili ya
kuwapatia burudani watumiaji wa umeme wa jua .
Mkuu
wa Mauzo na Masoko wa Mobisol Tanzania,Patrick Juma,amesema kuzinduliwa
kwa televisheni kubwa na ya kisasa katika soko la Tanzania ni
mwendelezo wa dhamira ya kampuni ya kutoa huduma bora za umeme wa
nishati ya jua , na kuuza bidhaa bora zinazotumia bidhaa hiyo.Aliongeza
kuwa tayari televisheni hiyo kubwa kuanzia sasa inapatikana katika vituo
vyote vya mauzo vya kampuni nchini kote.
Juma,
alisema bidhaa hii mpya inapatikana ikiwa imeunganishwa pamoja na
mtambo wa Sola Watti 200, kuhakikisha kuwa inafanya kazi kwa zaidi ya
masaa 10 ,pia inakuja nakifurushi chenye taa nne,redio na tochi-vyote
upatikanaji wake umewekwa katika mfumo unaowezesha wateja kumudu
kuzinunua kwa kulipia kidogo kidogo.Pia mteja atakayenunua televisheni
kubwa atanufaika kwa huduma mbalimbali ikiwemo kuunganishiwa
bure,atapata waranti na kuweza kuchagua huduma za televisheni ya kulipia
anayoitaka.Ofa hii kubwa kwa wateja yenye kuleta burudani kwa pamoja ya
matumizi ya vifaa vya kisasa vinavyotolewa na Mobisol kwa kushirikiana
na kampuni ya StarTimes.
Mkuu
wa Mauzo na Masoko wa Mobisol Tanzania,Patrick Juma anasema
“Tunajivunia kuendelea kuongoza kwa huduma na bidhaa zinazotumia umeme
wa jua zenye ubora na za kisasa na kufanikisha ndoto kubwa za watumiaji
wa umeme wa nishati ya jua,hususani wamiliki wa biashara na kwa matumzi
ya nyumbani sehemu za mijini ambao wanahitaji bidhaa kwa kadri ya
matumizi yao na mitindo yao ya maisha.Televisheni sio kifaa cha burudani
tu bali pia kinawezesha kupata maarifa sambamba na kuingiza kipato kwa
wanaokitumia kibiashara iwe kwenye mabaa,migahawa,mashuleni na vituo vya
elimu,na kwa matumizi ya kifamilia.’’
Pia Televisheni hii ya Inchi 43 imepata kuthibitishwa kimataifa na kampuni ya Lighting Global yenye dhamana ya kuhakikisha ubora wa hali ya juu katika mitambo na vifaa vya sola vinavyotengenezwa.
Mobisol mpaka sasa imefanikiwa
kuweka umeme wenye nguvu za 10MW na kuunganisha familia zaidi ya
500,000 kwenye mtandao wake katika kanda ya nchi za Afrika Mashariki kwa
gharama nafuu,ubora wa hali ya juu na unaowezesha matumizi ya
kibiashara.Kwa umeme wake wa ukubwa kuanzia mitambo ya Watii 40 mpaka
Watti 200,Mobisol imewezesha matumzi ya umeme kuanzia kuwasha
taa,kuchaji simu,pia matumizi ya vifaa vikubwa ,bora na vya kisasa
vinavyotumia umeme wa jua kama redio, Mobichaja na Televisheni.
No comments :
Post a Comment