Afisa usimamizi wa fedha kutoka
TAMISEMI Bw.Elisa Rwamiago akifungua mafunzo ya Mfumo wa Usimamizi wa
fedha za Umma toleo la 10.2 (Epicor 10.2) kwa wahasibu na Waweka hazina
wa Halmashauri za Iringa, Tanga,Morogoro na Kilimanjaro leo Mkoani
Iringa.Kulia kwake ni Mtaalamu Mshauri wa masuala ya rasiliamali fedha
kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) Bi Hellen
Nyagwa na wa kwanza kushoto ni Meneja wa Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo
ya Sekta za Umma (PS3) Mkoa wa Iringa Bw.Baraka Mwambene.
Mtaalamu Mshauri wa masuala ya
rasiliamali fedha kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma
(PS3) Bi Hellen Nyagwa akielezea ufanyaji kazi wa Mradi wa Uimarishaji
wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Mfumo
wa Usimamizi wa fedha za Umma toleo la 10.2 (Epicor 10.2) kwa wahasibu
na Waweka hazina wa Halmashauri za Iringa, Tanga,Morogoro na Kilimanjaro
leo Mkoani Iringa.Kulia kwake ni Afisa usimamizi wa fedha kutoka
TAMISEMI Bw.Elisa Rwamiago.
Wahasibu na Waweka hazina wa
Halmashauri za Iringa, Tanga,Morogoro na Kilimanjaro wakifuatilia
mafunzo ya mfumo wa Usimamizi wa fedha za Umma toleo la 10.2 (Epicor
10.2) leo Mkoani Iringa.
Mhasibu kutoka Ofisi ya
Rais-TAMISEMI Bw.Juma Shaha akielezea umuhimu wa matumizi ya mfumo wa
Usimamizi wa fedha za Umma toleo la 10.2 (Epicor 10.2) kwa wahasibu na
Waweka hazina wa Halmashauri za Iringa, Tanga,Morogoro na Kilimanjaro
leo Mkoani Iringa.
Picha zote na Daudi Manongi,MAELEZO,IRINGA
No comments :
Post a Comment