Wednesday, April 25, 2018

PROF.MUSERU:AWATAKA WAFANYAKAZI HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI WAENDELEE KUTOA HUDUMA BORA KWA WAGONJWA

????????????????????????????????????
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Prof. Lawrence Museru akiongoza kikao cha Baraza la Wafanyakazi la hospitali hiyo jana. Kushoto ni Katibu Msaidizi wa baraza hilo, Merina Rwechungura  na kulia ni Katibu wa Baraza hilo, Elineza Msuya.
002
Wajumbe wakipitia makabrasha kwenye mkutano huo.
003
Mwakilishi wafanyakazi wa hospitali hiyo, Judith Nyaruga akichangia mada kwenye mkutano huo jana.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wajumbe wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa na wawakilishi wa wafanyakazi.
005
Mmoja wa wajumbe wa baraza hilo, Deus Buma akichangia mada kwenye mkutano huo.
006
Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho.
…………….
Wafanyakazi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakiwamo madaktari na wauguzi wametakiwa kuendelea kutoa huduma bora kwa wagonjwa na kwamba atakayekwenda kinyume na agizo hilo atachukuliwa hatua na mamlaka husika.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Prof. Lawrence Museru kwenye kikao cha Baraza la Wafanyakazi ambako kulijadiliwa mambo mbalimbali yakiwamo
huduma bora kwa wagonjwa, mafanikio, maslahi kwa wafanyakazi na mikakati ya kujenga miundombinu mipya na kukarabati ile ya zamani.
Katika mkutano huo Prof. Museru amewataka wafanyakazi kutoa taarifa za watumishi wenzao wanaotoa huduma zisizoridhisha kwa wagonjwa pamoja na wateja wengine wanaofika MNH kwa ajili ya kupatiwa huduma.
“Watumishi watakaotajwa kwamba wanatoa huduma mbaya kwa wagonjwa na wateja wengine watachukuliwa hatua, lengo ni kuboresha huduma za afya,” amesema Prof. Museru.
Prof. Museru amewasisitiza wafanyakazi kutoa ushirikiano katika mikakati inayoendelea ya kutoa huduma bora za kibingwa ikiwamo upandikizaji wa figo, upandikizaji wa vifaa vya usikivu kwa watoto wasiosikia na huduma mbalimbali za kibingwa.
Mkurugenzi huyo amewaeleza wafanyakazi kwamba hospitali inaendelea kutoa huduma bora za kibingwa ikiwamo upandikizaji wa figo na vifaa vya usikivu kwa watoto.
Amesema hospitali ilifanikiwa kupandikiza figo kwa mgonjwa mmoja na changamoto zilizojitokeza tayari zimefanyiwa kazi na hivyo kuwezesha wagonjwa wanne kupandikizwa figo mwezi huu na kwamba kila mwezi wagonjwa watano watakuwa wakipandikizwa figo.
“Hospitali inaendelea kuboresha miundombinu inayotumika wakati wa upasuaji wa kupandikiza figo na baada ya maboresho haya kila siku mgonjwa mmoja atakuwa akipandikizwa figo.
Katika hatua nyingine, Prof. Museru amesema huduma ya upandikizaji vifaa vya usikivu inaendelea vizuri na kwamba mwishoni mwa mwezi wa tano au wa sita mwanzoni wagonjwa watano watapandikizwa vifaa vya usikivu na kwa mwaka wagonjwa 24 watakuwa wamepatiwa huduma hiyo.
Amesema pia hospitali ipo kwenye mikakati ya kujenga jengo jipya ambalo litatumika kulaza wagonjwa na kutoa huduma  mbalimbali ikiwamo upandikizaji wa figo.
Naye Mkurugenzi wa Fedha wa Hospitali hiyo, Gerald Jeremiah amewataka wafanyakazi hao kujenga tabia ya kufuatilia michango yao sehemu husika ili kuweka taarifa vizuri ya mafao yao kabla ya kustaafu.

No comments :

Post a Comment