Friday, March 2, 2018

VIDEO:UJUMBE KUTOKA WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MACHI,08,2018.



Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, tunapenda kuwafahamisha wanawake, jamii na wadau wengine kuwa Maadhimisho ya Mwaka huu yatafanyika katika ngazi ya Mikoa.
Kaulimbiu ni “Kuelekea Uchumi wa Viwanda: Tuimarishe Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji Wanawake Vijijini”. Kupitia kaulimbiu hii wadau wote tunaaswa kuongeza kasi ya kuwezesha kufikiwa kwa usawa wa jinsia na kuwawezesha wanawake wa vijijini kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali katika kuelekea uchumi wa kati na wa viwanda.

No comments :

Post a Comment