Wednesday, March 21, 2018

POLISI YAKAMATA 58 NA GRAMU 74 ZA HEROIN KATIKA OPERESHENI YA DAWA ZA KULEVYA


c253346c5ae17ee8722c08eac00cfe30
  1. UTANGULIZI ;
    Zipo taarifa kuwa baadhi ya wananchi Mkoa wa Mjini Magharibi wanatumia, wanashiriki, wanafadhili au kusaidia biashara ya madawa ya kulevya kama ilivyo kwenye maeneo mengine nchini.  
Hata hivyo Serikali ipo kwenye vita kali ya kupambana na mtandao wa madawa ya kulevya na Inspekta Jenerali wa Polisi kwa kushirikiana na Kamisheni ya Polisi Zanzibar waliunda timu kutoka Kitengo cha Operesheni Maalum za Polisi Makao Makuu Dar es salaam kuja kuongeza nguvu katika ufuatiliaji wa kero hii kama ilivyo kwenye maeneo mengine ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
  1. MATOKEO YA OPERESHENI ;
S/N MAFANIKIO MATOKEO / IDADI
TAARIFA ZA INTELIJENSIA

Kupatikana kwa taarifa za  watuhumiwa wanaojihusisha na mtandao wa madawa ya kulevya (kutumia, kuuza, kufadhili au kusaidia) 105
JUMLA KUU 105
WATUHUMIWA  WALIOPATIKA NA HATUA

Watuhumiwa waliofikishwa Mahakamani 26

Watuhumiwa waliopo chini ya Upelelezi 16

Watuhumiwa waliopo chini ya uangalizi wa Polisi (Police Supervisee) 16
JUMLA KUU 58
VIELELEZO

Heroin   Kete 1293 na Vifuko 3 sawa na Gramu 74.385

Banghi (Vifurushi) 373

Banghi (Vifuko) 3
  1. WITO :
    Natoa wito na tahadhari kwa wananchi wote wanaohusika kwenye mtandao huu kuacha mara moja kwa kuwa vita hii imeshaanza na inaendelea kwa lengo la kuhakikisha usalama wa vizazi vilivyopo na vizazi vijavyo maana madawa haya yanaathiri zaidi vijana ambao ndiyo muhimili na nguvu kazi ya Taifa.
Aidha nawapongeza wananchi wote waliotoa ushirikiano wa kutoa taarifa za uhalifu huu bila ya kuona muhali. Niwaombe wananchi wote kuendelea na ushirikiano huu wa kutoa taarifa.
Mwisho natuma salamu kwa watuhumiwa wote waliotoroka kule walipo wajue kuwa wanatafutwa na watakamatwa ili wahojiwe na hatimae kufikishwa Mahakamani.
Ahsanteni sana kwa kunisikiliza
Liberatus Sabas – DCP
Mkuu Wa Uperesheni Maalum za Polisi Tanzania
21.03.2018

No comments :

Post a Comment