Sunday, March 18, 2018

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI YATEMBELEA KIWANDA CHA TBL- MWANZA


KAMATI YA BUNGE TBL 2 KAMATI YA BUNGE TBL 4
Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, wakiangalia bia inavyopikwa katika kiwanda cha bia TBL tawi la  Mwanza, walipotembelea jijini huo jana.
KAMATI YA BUNGE TBL 7 KAMATI YA BUNGE TBL 11
Wajumbe wa kamati ya Bunge wakitembea maeneo mbalimbali ya kiwanda
KAMATI YA BUNGE TBL 13
Mkurugenzi wa kiwanda cha Konyagi(TDL|) Devis Deogratius akiwasilisha mada ya utendaji wa kampuni ya bia TBL kwa  Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, walipotembelea kiwanda cha jijini Mwanza
KAMATI YA BUNGE TBL 15
Meneja wa kiwanda cha bia TBL tawi la Mwanza Marietha Mazula, akifafanua jambo kwa  Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, walipotembelea kiwanda hicho jijini Mwanza
……………….
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti mwishoni mwa wiki ilitembelea kiwanda cha kutengeneza Bia cha TBL cha Mwanza kilichopo chini ya kampuni ya TBL Group ambapo waliweza kutembelea vitengo  mbalimbali vya uzalishaji sambamba na kupata maelezo jinsi  kiwanda kinavyoendeshwa.
 
Meneja wa TBL Mwanza,Marietha Mazula,aliwaeleza wajumbe  wa kamati hiyo mikakati mbalimbali ambayo inafanywa na kampuni ya  TBL Group kuhakikisha inaimarika zaidi  katika kufanikisha kwa vitendo mkakati wa serikali ya awamu ya tano ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
Baadhi ya mikakati ambayo kampuni imeanza kutekeleza aliitaja kuwa ni kuwekeza katika kutumia teknolojia za kisasa katika uzalishaji sambamba na kuwezesha wakulima wanaoiuzia kampuni malighafi ili kuhakikisha kukua kwa viwanda kunakuza sekta ya kilimo pia na kupunguza tatizo la ajira nchini.

No comments :

Post a Comment