Na Florah Raphael.
Benki kuu ya dunia kwa kushirikiana na Wizara ya maji na
umwagiliaji Tanzania wamekutana leo jijini Dar es salaam kujadili
miundombinu na miradi bora ambayo itawapatia watanzania maji safi na
salama, ambapo tangu mwaka 2006-2017 katika mpango wa kuboresha vyanzo
vya maji Tanzania imefanikikiwa kujenga miradi ya maji 1468 badala ya
10810 na vituo vya kuchotea maji 123,888 huku vinafofanya Kazi vikiwa ni
83331 na 38602 vikiwa havifanyi Kazi, katika mkutano huo benki ya dunia
imeahidi kuchangia milioni 300 kwa ajili ya mradi wa maji vijijini.
Akiongea na vyombo
vya habari naibu waziri wa maji na umwagiliaji amesema kuwa kutokana na
mafanikio hayo bado kuna changamoto kubwa katika ujenzi wa miradi hiyo
kwani wahandisi wengi ni kutoka nje ya nchi na hawayafahamu vizuri
mazingira ya Tanzania hivyo inapelekea kujenga miradi mingi ambayo kwa
badae inakuwa haina maji hivyo inabaki kuwa hasara.
Hata hivyo amekanusha
kwamba siyo kwamba hawataki wahandisi wageni bali wanawataka kuwa na
ushirikiano na wahandisi wenyeji kwani wao ndio wanaijua vizuri
geografia ya nchi yao na wanafahamu wapi panatoa maji na wapi hapatoi
maji hata wakati wakiangazi.
” siyo kwamba
hatutaki waje nchini hapana lakini wanatakiwa kuwasikiliza wenyeji wao
kwani wakija hapa nchini wao wanakuwa na sauti kuliko wenyeji” amesema.
Kamwelwe.
Aidha amesema kuwa
changamoto nyingine ni teknolojia hasa kwa vijijini kwani miradi mingi
vijijini imekuwa ikiendeshwa kwa diezeli hivyo kugharimu watumiaji
gharama kubwa na matokeo yake kushindwa kumudu na hatimaye kukosa
kutumia maji yaliyo salama na kuendelea kutumia maji ya madimbwi ambayo
ni hatari kwa afya zao na kueleza kuwa kwa sasa watabadilisha
miundombinu hiyo na kuifanya iweze kutumia umeme wa jua.
Amesema pia Wizara
imejipanga kuwa na Sera na sheria ili serikali iweze kutoa bajeti ili
kuweza kuboresha miundombinu ya maji taka na kuweza kujenga mitambo ya
kutibu maji taka ambapo ameweka wazi kwamba wafadhili mbalimbali
wameanza kujitokeza kufadhi, benki kuu ya dunia imetoa pesa ambayo
itatumika kujenga mtambo wa kutibu maji taka mbezi bichi, Wakolea
wametoa pesa itakayojenga mtambo kama huohuo maeneo ya jangwani na
Kurasini ambapo tayari mtambo huo umeshajengwa na umefadhiliwa na benki
ya maendeleo ya Afrika.
No comments :
Post a Comment