Friday, January 26, 2018

KATIBU MKUU RWEGASIRA, AIAGIZA TBA KUMALIZA UJENZI NYUMBA ZA ASKARI MAGEREZA KWA WAKATI


PIX 1
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu, Projest Rwegasira akimsalimia Kaimu Meneja wa Mkoa wa Dar es Salaam, Wakala wa Majengo nchini (TBA-B), Manasseh Slekelaghe (Kushoto), mara baada ya Katibu Mkuu huyo kumaliza ziara yake ya ukaguzi wa ujenzi wa nyumba za askari Magereza, zilizopo Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Katibu Mkuu huyo aliiagiza TBA kumaliza ujenzi huo kwa muda wa miezi mitano kuanzia sasa.
PIX 2.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu, Projest Rwegasira (wapili kushoto) akimsikiliza Mratibu wa Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Askari Magereza, Mhandisi Khadija Salum, alipokua anamuonyesha Katibu Mkuu huyo maeneo mbalimbali ya ujenzi wa nyumba hizo zilizopo Ukonga, jijini Dar es Salaam. Katibu Mkuu huyo aliiagiza TBA kumaliza ujenzi huo kwa muda wa miezi mitano kuanzia sasa.
PIX 3
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu, Projest Rwegasira (katikati) akimsikiliza Msimamizi wa Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Askari Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Magereza, Cosmas Mtambala (kushoto), alipokua akimuonyesha Katibu Mkuu huyo hatua mbalimbali za ujenzi wa nyumba hizo zilipofikia. Katibu Mkuu alifanya ziara ya kuzitembelea nyumba hizo, zilizopo Ukonga,jijini Dar es Salaam, kuangalia ujenzi unavyoendelea. Katibu Mkuu huyo aliiagiza TBA kumaliza ujenzi huo kwa muda wa miezi mitano kuanzia sasa.
PIX 4
Moja ya jengo la Makazi ya Askari Magereza likionekana hatua iliyofikia. Nyumba hizo zilizopo Ukonga jijini Dar es Salaam, zinajengwa na Wakala wa Majengo nchini (TBA-B) na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini. Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, aliiagiza TBA, kumaliza ujenzi wa nyumba hizo kwa muda wa miezi mitano kuanzia sasa.
PIX 5
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu, Projest Rwegasira akiwafafanulia jambo wajenzi wa Nyumba za Askari Magereza zilizopo Ukonga jijini Dar es Salaam, ambao ni Wakala wa Majengo nchini (TBA-B).  Kushoto (meza kuu) ni Kaimu Meneja wa Mkoa wa Dar es Salaam (TBA-B), Manasseh Slekelaghe, anaefuata ni Mratibu wa Mradi wa Ujenzi wa Nyumba hizo, Mhandisi Khadija Salum, na kushoto ni Mhandisi wa Mradi huo, Peter Kikwati. Kulia ni Msimamizi wa Mradi wa huo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Magereza, Cosmas Mtambala. Katibu Mkuu alizikagua nyumba hizo leo na kutoa muda wa miezi mitano ziwe zimekamilika.
PIX 6
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu, Projest Rwegasira akiwafafanulia jambo wajenzi wa Nyumba za Askari Magereza zilizopo Ukonga jijini Dar es Salaam, ambao ni Wakala wa Majengo nchini (TBA-B), pamoja na wasimamizi wa mradi huo ambao ni Maafisa wa Jeshi la Magereza.  Kushoto (meza kuu) ni Kaimu Meneja wa Mkoa wa Dar es Salaam (TBA-B), Manasseh Slekelaghe. Katibu Mkuu alizikagua nyumba hizo leo na kuiagiza TBA kumaliza ujenzi wa nyumba hizo kwa muda miezi mitano kuanzia sasa.
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments :

Post a Comment