Tuesday, November 21, 2017

TANZANIA YAPIGWA MSASA NA ISRAEL WA KUTANGAZA UTALII KIDIGITALI

1
Dr. Noam Koriat akitoa mafunzo kwa watumishi wa Wizara ya Utalii na Taasisi zake katika ukumbi wa mikutano wa Makumbusho ya Taifa, jijini Dar es salaam.
2
Baadhi ya Watumishi wakimsikiliza Dkt. Wakati wa mafunzo.
…………..
Ziara  ya kutembelea nchi ya Israel iliyoandaliwa na Bodi ya Utalii Tanzania na kuhususisha viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii imeanza kuzaa matunda ambapo mtaalamu wa mfumo wa mawasiliano Kutoka Israel, Dkt Norma Kortiat amewasili nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo yanayohusiana na jinsi ya kutangaza utalii wa Tanzania kwa njia ya kidigitali “Digital Marketing”. Mafunzo haya yanategemewa kuwawezesha watumishi  kuongeza ufanisi kwa wa kutumia teknologia mpya katika kuvitangaza vivutio vya utalii vya Tanzania.
Mafunzo haya ya siku mbili yameanza leo tarehe 21-22 yanafanyika katika ukumbi wa mikutano wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam ambayo  yanahudhuriwa na watumishi Kutoka Idara ya Utalii , Bodi ya Utalii, Mamlaka ya Wanyama Pori,Mamlaka ya Hifadhi za Taifa, Mamlaka ya Bonde la Ngorongoro, Wakala wa Huduma za Misitu na kamisheni ya Utalii Zanzibar.

No comments :

Post a Comment