Friday, October 20, 2017

RC APIGA MARUFUKU UTOAJI WA LESENI ZA UCHIMBAJI WA MADINI AMANI MUHEZA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella kushoto akimtwisha ndoo mkazi wa eneo hilo kuashiria uzinduzi wa mradi wa maji wa kwanza kulia ni Kaimu  Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Tanga,Mhandisi Laurian Rwebembeza kushoto  ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mhandisi Robert Gabriel

 MKUU wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella akizungumza wakati wa uzinduzi wa Jumuiya Tatu za Zigi Juu,Zigi Chini na Kuhuhwi zilizopo kwenye Bonde la Mto Pangani katika eneo Amani wilayani Muheza na mradi wa maji mserereko kwa ajili ya vijiji vya Mashewa,Kimbo na Shembekeza
 MKUU wa wilaya ya Muheza,Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mhandisi Robert Gabriel
 MKUU wa wilaya ya Korogwe,Mhandisi Robert Gabriel akizungumza katika uzinduzi wa mradi huo
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza katika uzinduzi huo
Mwakilishi kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa  UNDP ambao wamefadhili mradi huo akizuungumza katika uzinduzi huo

Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Muheza akizungumza katika uzinduzi huo Jumanne Omari
 Mhifadhi wa Amani,Mwanaidi Kijazi kushoto akimuelekeza sehemu ambazo mazingira yameharibiwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella ambaye alitembelea eneo hilo juzi ambalo ni vyanzo vya maji limekuwa likitumiwa na wachimbaji wa madini ambapo serikali imetaka leseni zilizotolewa zifutwe
 Mhifadhi wa Amani,Mwanaidi Kijazi kushoto akimuelekeza sehemu ambazo mazingira yameharibiwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella ambaye alitembelea eneo hilo juzi ambalo ni vyanzo vya maji limekuwa likitumiwa na wachimbaji wa madini ambapo serikali imetaka leseni zilizotolewa zifutwe
 Baadhi ya maeneo yaliyoathirika kutokana na uchimbaji haramu wa madini katika eneo la Hifadhi ya Amani wilayani Muheza
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella akitembelea maeneo hayo kujionea athari ambazo zimetokana na uchimbaji haramu wa madini kwenye eneo la vyanzo vya Maji Amani na Hifadhi ya Msitu
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Jumuiya ya watumiaji wa Maji na Mradi wa Maji Mserereko kwa vijiji vya Masheww,Kimbo na Shembekeza wilayani Muheza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza,Mhandisi Mwanasha Tumbo na Katibu Tawala Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella katikati akizundua mradi huo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Muheza,Mhandisi Mwanasha Tumbo anayeshuhudia mwenye kilembe cheusi kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga(RAS) Mhandisi Zena Saidi
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella kushoto akiteta jambo na Mkuu wa wilaya ya Muheza,Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Said

Sehemu za wananchi wakishuhudia uzinduzi huo
MKUU wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella ameitaka wizara ya Madini kuacha kuendelea kutoa leseni za uchimbaji wa madini eneo hifadhi ya Amani wilayani Muheza huku wakitaka zilizotolewa kufutwa kutokana na uharibifu wa mazingira unaoendelea kwenye eneo hilo.

Kwani uchimbaji huo umekuwa na madhara makubwa kuharibu mazingira kutokana na kutumia kemikali  ambazo huingia kwenye... maji na hivyo kuleta adhari kubwa kwa binadamu ambayo huyatumia kwa matumizi mbalimbali.

Aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Jumuiya za watumiaji maji Bonde Dogo la Mto Zigi katika Uzinduzi wa Jumuiya tatu za Zigi Juu,Zigi Chini na Kihuhwi zilizopo Bonde la Pangani.

Mradi huo wa Maji wa Mserereko ulihusisha vijiji vya Mashewa,Kimbo na Shembekeza wilayani Muheza Mkoani Tanga.

Alisema pia licha ya kupiga marufuku hiyo lakini watahakikisha wanawachukulia hatua watumishi watakaoshirikiana na wachimbaji kwa kuwakamata na kuwapeleka kwenye vyombo vya dola ili kuweza kukomesha tatizo hilo.

“Labda nisema tu sisi kama mkoa tumepiga marufuku uchimbaji wa madini katika eneo hili la Amani lakini pia tunaitaka Wizara ya Nishati wasiendelea kutoa leseni za madinina mtu atakayekwenda kuchukua leseni hela yake  itakuwa imeibiwa”Alisema  

“Lakini pia niseme pia kwa wale ambao leseni wamepewa zifutwe kwani kuendeleza uchimbaji huo kunaweza kusababisha madhara makubwa sana kwa uharibifu wa mazingira “Alisema.

No comments :

Post a Comment