Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya
Mawasiliano nchini James Kilaba (katikati) akiandika maoni ya wadau wa
mitandao ya blogu na Online Tv wakati wa uzinduzi wa kampeni ya
kusisitiza matumizi bora ya mitandao ya kijamii kwa awamu ya pili mapema
hii leo jijini Dar es Salaam.
…………….
Na. Paschal Dotto-MAELEZO.
22/09/2017
Serikali ya Awamu ya Tano kupitia
Mamlaka ya Mawasiliano nchini(TCRA) imetia nia kuboresha mawasiliano kwa
umma hasa katika matumizi ya mitandao ya kijamii ili kuwawezesha
watanzania kupata elimu bora ya...
maendeleo na kujenga uchumi uliobora.
Haya yamesemwa leo Jijini Dar es
Salaam na Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka hiyo Dkt. Jonas Kilimbe
alipokua akihutubia hadhara ya wamiliki wa vyombo vya habari mtandaoni
(blogu na Online TV) katika uzinduzi wa kampeni ya awamu ya pili ya
“kusisitiza matumizi bora ya mitandao ya kijamii” iliyofanyika katika
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
Katika hafla hiyo, Dkt. Kilimbe
alisema kuwa kwa sasa teknolojia ya mtandao inakua kwa kasi kwa hiyo
huduma za habari zinapatikana kila sehemu kwa njia ya mtandao na kufanya
matumizi ya mitandao kuwa makubwa.
“Sekta ya mawasiliano kwa umma
imepiga hatua kubwa sana duniani kwa sasa, kwa kiasi kikubwa mtandao
unachangia kuwepo kwa habari nyingi. Tanzania inajumla ya televisheni za
mitadaoni zipatazo 50 pamoja na blogu 150 ambazo zote zinatoa taarifa
kwa wananchi, hii inaashiria kuwa mawasiliano kwa umma yamehamia zaidi
kwenye mtandao”, alisema Dkt.Kilimbe.
Aidha Dkt.Kilimbe alisema kuwa
sekta hii inapaswa kuangaliwa zaidi kwani ni sekta muhimu kwa ujenzi wa
Taifa na kuwaasa vijana kutumia vizuri teknolojia hiyo kwa kujielimisha
kuhusiana na masuala ya maendeleo kuliko kutumia vibaya mitandao hiyo.
“Tuna jukumu zito na ni kubwa kwa
sababu sekta hii ya mawasiliano imeshikiria kila kitu na tasnia ya
habari ina nguvu kubwa sana kwa kuleta elimu ya maendeleo kwa wananchi
kwa hiyo waandishi mitandaoni tumieni weledi mkubwa kwa habari za
maendeleo.”, alisisitiza Dkt. Kilimbe.
Dkt.Kilimbe alisema kuwa katika
matumizi ya teknolojia hii mpya yanapaswa kuzingatiwa kwa ajili ya
ujenzi wa taifa hasa kwa wale wanaotumia vizuri mitandao ya kijamii
inawapa elimu kubwa ya maendeleo.
Aidha Dkt. Kilimbe amekishukuru
chama cha wamiliki wa blogu na televisheni mtandaoni(TBN) kwa kuleta
umoja na kuzingatia maadili na weledi wa umilikajia wa vyombo hivyo kwa
kuwahabarisha wananchi.
Naye mtoa mada na mwakilishi
kutoka TCRA Bw. Thadeus Lingo alisisitiza usalama wa matumizi ya mtandao
akisema kuwa idadi ya watumiaji wa mitandao imeongezeka duniani kuanzia
Julai 1, 2017 na kufikia bilioni 3.8 huku kati ya hao bilioni 3.4
ambayo ni sawa na asilimia 92 ni watumiajia wa mitandao ya kijamii hali
iliyosababisha kuongezeka kwa vyombo vya habari kuhamia mtandaoni, kwa
hiyo weledi unahitajika katika kuhabarisha umma kwa njia hii.
No comments :
Post a Comment