Wednesday, May 10, 2017

WAMILIKI WA SHULE YA LUCKY VINCENT WAKAMATWA NA POLISI



Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha ( RPC ), Charles Mkumbo amesema wanamshikilia mmiliki wa basi dogo aina ya Coaster ambayo ilipata ajali na kusababisha vifo kwa wanafunzi, walimu na dereva wa shule ya  Lucky Vincent iliyoko Kwa-Mrombo kata ya Olasiti jijini Arusha
Kamanda Mkumboamesema pia Polisi inamshikilia mmiliki wa shule hiyo kwa kuruhusu gari yake hiyo kubeba abiria wengi zaidi kuliko uwezo wake.
"Siku ya tukio walikuwepo abiria 38 kwenye gari katika uchunguzi baada ya kubaini hilo tumeshachukua hatua kwa mtu aliyewezesha gari hilo kupakia hao watu, tumeshamkamata mmiliki wa gari ambaye ndiye mwenye shule hii, sasa hivi tunaendelea na uchunguzi na utakapokamilika atafikishwa mahakamani" alisema RPC wa Arusha.
Kwa mujibu wa Mkumbo anasema gari hiyo ilikuwa na kibali cha kubeba watu 30 lakini siku ya ajali ilikuwa na watu zaidi ya 30.

Aliekuwa Mkuu wa wilaya ya Lindi, Yahaya Nawanda, (katikati), akikata utepe kuzindua mradi wa”Hakuna wasichoweza” unaowapatia elimu ya hedhi na vifaa vya kujistiri wasichana ili wasikose kuhudhuria masomo yao mashuleni, Mradi huo unadhaminiwa na Vodacom Tanzania Foundation na kuendeshwa na T-Marc Tanzania mkoani humo,Wengine katika picha kutoka kushoto ni Aisha Mahadni mwanafunzi wa shule ya msingi stadium,Renatus Rwehikiza aliekuwa mkuu wa Vodacom Tanzania Foundation,Mkurugenzi wa T-Marc Tanzania,Diana Kisaka na Lalat Saidi.

No comments :

Post a Comment