Friday, April 21, 2017

TANZANIA YAJIZATITI KUHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI PWANI YA BAHARI YA HINDI.

8235417469_ea7a0e3ee7_b
                        Na. Lilian Lundo – MAELEZO
Mabadiliko ya Tabianchi ni moja ya eneo ambalo limekuwa likileta athari kubwa katika nchi nyingi Duniani
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zimeweka mikakati mbalimbali katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Moja ya mikakati hiyo ni pamoja na ujenzi wa kuta kwenye Pwani ya Bahari ya Hindi, upandaji wa mikoko ikiwa ni pamoja na uchimbaji wa mifereji ya maji ya mvua na maji machafu
Akitoa taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, Mkurugenzi Idara Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais, Richard Muyungi anasema Mradi wa
kujenga uwezo wa kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi katika Pwani ya Bahari ya Hindi jijini  Dar es Salaam unatekelezwa katika maeneo manane na unagharimu dola za kimarekani milioni tano..
Bwana Muyungi anasema maeneo ambayo mradi huo unatekelezwa kuwa ni eneo la Obama Ocean Road, Kigamboni kwenye Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere, Bungoni Ilala, Miburani Mtoni, Temeke, Salender Bridge, Kunduchi, Mbweni na Ununio Kinondoni.
Anasema jumla ya Dola za Marekani 3,489,482 zimetengwa  kwa ajili ya miundombinu ya ujenzi wa ukuta eneo la  Ocean Road na Kigamboni pamoja na mitaro iliyopo Bungoni, Ilala na Mtoni Temeke
Katika ziara hiyo Bwana Muyungi anazitaja shughuli nyingine zinazotekelezwa katika mradi huo ni pamoja na kukarabati ukuta wa bahari katika maeneo ya barabara ya Obama ambayo zamani ilijulikana kama Ocean Road wenye  urefu wa mita 820  na Kigamboni eneo la Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere, urefu wa mita 380, ambapo ukuta huo utadumu kwa zaidi ya miaka 73.
Pamoja na matengenezo hayo, fedha nyingine zitatumika kutoa mafunzo kuhusu nishati safi ya kurudisha mikoko ekari 40 ya mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi katika maeneo ya Jiji la Dar es Salaam.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA), Sheha Mjaja anaeleza miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni pamoja na  mradi wa kujenga uwezo wa kuhimili athari za mabadiliko ya Tabianchi katika maeneo ya ukanda wa Pwani (mradi wa LDCF).
 “Mradi huu unatekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ofisi ya makamu wa Rais katika maeneo ya Bagamoyo, Pangani, Rufiji na Zanzibar na unafadhiliwa na Mfuko wa Dunia wa Mazingira (The Global Environmental Facility- GEF) kupitia dirisha la Mfuko wa Nchi Masikini Duniani (The Least Developed Countries Fund – LDCF) la Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi – UNFCCC,” anafafanua Sheha Mjaja.
Anafafanua kuwa fedha za Mradi huo zinapitia Shirika la Usimamizi wa Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) ambalo pia lina jukumu la kutoa ushauri wa kitaalamu na usimamizi wa fedha na Jumla ya Dola za Kimarekani milioni  3,356,300 zimepangwa kutumika katika mradi huu zikijumuisha fedha za usimamizi na ufuatiliaji za UNEP ambapo Utekelezaji wa Mradi huu ulianza mwaka 2013 na unategemewa kumalizika mwaka 2017.
Mkurugenzi mkuu huyo wa ZEMA amezitaja shughuli zitakazofanyika katika mradi huo ni upandaji wa mikoko/mikandaa na miti ya ukanda wa pwani katika maeneo 6 ya Unguja na Pemba pamoja na ujenzi wa kuta za bahari katika eneo la Kilimani mjini Unguja na Kisiwa Panza, wilaya ya  Mkoani Pemba.
Anafafanua kuwa, eneo la Kilimani ambalo ufukwe wake una urefu wa mita 538 litajengwa kuta mbili (2) za aina ya “gyrones”,ambapo kila ukuta  utakuwa na urefu wa mita 100 kutoka kwenye fukwe kuelekea

No comments :

Post a Comment